• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

AHADI ZA MAKAMU WA RAIS Mhe. Dkt. PHILIP ISDORI MPANGO WA WANANCHI WA JIMBO LA ARUMERU MAGHARIBI....

Posted on: May 18th, 2023

Na ElinipaLupembe

Makamu wa Rais Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Isdori Mpango, ametoa maagizo kwa Mamlaka husika kupitia Mawaziri wenye dhamna kutatua kero  zinazowakabili wananchi wa halmashauri ya Arusha, zilizowasilishwa Mbunge wa Jimbo la Arumeru Magharibi Mhe. Noah Lembis Saput.

Hata hivyo Mhe. Dkt. Mpango ametoa pole kwa wahanga wote wa changamoto hizo na  kumuagiza Mkurugenzi wa TARURA nchini kusimamia matengenzo ya barabara za ndani za zilizoharibiwa na mvua kubwa zilizonyesha katika msimu huu wa mvua zikikata mawasiliano kwa baadhi ya maeneo na kusababisha adha kubwa kwa wakazi wa maeneo hayo.

Aidha amemuagiza Meneja wa TARURA mkoa wa Arusha kuangalia salio la bajeti na kudhibiti korongo lililo pembeni ya kanisa Katoliki Ngaramtoni, korongo linalotishia usalama wa jengo hilo na waumini wa kanisa hilo.

Dkt Mpango ameiagiza Mamlaka ya Chakula NFRA kuangalia upya namna ya kuenendelea kutoa chakula cha ruzuku kwa watu wenye uhaba wa chakula, changamoto iliyosababishwa na ukame uliyakabili eneo kubwa katika jimbo hilo.

Kadhalika, amemtaka pia Waziri wa Maji kwa kushirikina na Mkurugenzi wa RUWASA kuongeza nguvu ya kusimamia miradi ya maji katika jimbo hilo, miradi ambayo imetaarifiwa na Mhe. Mbunge huyo kutekelezwa kwa muda mrefu bila kukamilika.

Na mwisho kabisa, amemuagiza Waziri mwenye dhamana TAMISEMI kufanyia kazi ombi la kuigawa wilaya ya Arumemeru kutokana na ukubwa wa eneo hilo na wananchi kupata adha ya kufika ofisi ya mkuu wa wilaya na kupata huduma, ombi ambalo lilitolewa na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Arusha, Comredi Steven Zelothe Steven.

"Kuna gharama kubwa katika kugawa na kuongeza maeneo ya kiutawala, lakini Mkoa na TAMISEMI fanyieni kazi upya na kuangalia uwezekano wa kugawa wilaya hiyo kwa dharura kwa kuzingatia vigezo vinavyohitajika kuwa wilaya" Amefafanua Mhe. Dkt. Mpango

Awali akizungumza wakati wa kutoa salamu za wananchi wa Jimbo la Arumeru Mh. Noah licha ya kuishukuru serikali ya awamu ya sita chini ya uongozi imara wa Jemadari mama Dkt. Samia Suluhu Hassani, amezitaja changamoto kubwa zinawazokabaili wananchi wa jimbo hilo ikiwa ni pamoja na uharibifu mkubwa wa barabara za ndani, uliotokana na mvua kubwa zilizonuesha katika msimu huu wa mvua, utekelezaji wa miradi ya maji kuchukua muda mrefu kukamilika na kusababisha wananchi kokosa maji kama yalivyo malengo ya serikali ya kufikisha asilimia 90 mijijini na  80 vijijini huku jimbo hilo likiwa na 65 tu.

Aidha Mhe. Noah amemuomba Makamu wa Rais, kutokana na hali ya ukame unayolikabili jimbo hilo, ameomba kuangalia upya namna ya kuendelea kuwapa chakula wananchi wa baadhi ya kata zilizokumbwa na ukame na kusababisha upungufu mkbwa wa chakula kwa baadhi ya wananchi.


ARUSHA DC ni Yetu, Tushirikiane Kuijenga"

KaziInaendelea





Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.