• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

ARUSHA DC YAWASHUKURU WADAU WALIOCHANGIA MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU 2022

Posted on: August 11th, 2022

Na Elinipa Lupembe

Uongozi wa halmashauri ya Arusha, umekabidhi vyeti vya pongezi na shukurani kwa wadau wa maendeleo wa halmashauri hiyo, walioshiriki kuchangia utekelezaji wa shughuli mbalimbali za utekelezaji wa miradi ya maendeleo wakati wa mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2022.

Akizungumza wakati wa kukabidhi vyeti vya pongezi, Mwenyekiti halmashauri ya Arusha, mheshimiwa Ojung'u Salekwa, amewashukuru wadau hao kwa ushirikiano na  kujitoa kwa moyo kuunga mkono juhudi za serikali kwa kuchangia utekelezaji wa miradi ya maendeleo kisekta wakati halmashauti ikiwa kwenye maandalizi ya mapokezi ya Mwenge wa Uhuru 2022.

"Serikali inatambua na kuthamini sana michango ya wadau wa maendeleo kwa kuwa wanafanya kwa niaba ya serikali, shukrani tuliyoitoa haina thamani ya huduma mliyoitoa, ila tunaamini katika utoaji wenu wenye baraka, maandiko yanasema heri mkono unaotoa kuliko kupokea" Amesisitiza Mheshimiwa Ojung'u

Hata hivyo mkurugenzi mtendaji, halmashauri ya Arusha, Seleman Msumi, licha ya kuwashukuru wadau hao kwa kuunga mkono juhudi za serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kwa maendeleo ya wananchi wa halamshauri ya Arusha na kwa taifa na kuwataka wasichoke kuendelea kuisaidia halmashauri hiyo kwa kuwa bado kuna mahitaji mengi ya kijamii ambayo serikali peke yake haiwezi kuitekelza.

Aidha Mkurugenzi Msumi, amewataja wadau hao ni pamoja na Mchungaji Philemon Olais  Mollel, Michael Lembris  Mollel, Eliaman Joseph Mollel, Olais Nanaya Mollel, Elibariki Kiberenge Levoyo,  Diwani wa kata ya Sokon II Mhe. Elias Long'idare Mollel, Remmy William Mollel, Julius Logiru Meshuko, pamoja na shirika la Walking in Love na shirika la CWCD.

Hata hivyo wadau hao wameushukuru uongozi wa halamsahuri kwa kutambua na kuthamini michango yao na kuahidi kuendelea kushirikiana na serikali ya awamu ya sita kuchangia maendeleo ya nchi.

Mchungaji Philemon Molel ameweka wazi kuwa, kwa halmashauri kutambua na kuthamini mchango walioutoa inajenga matumani na moyo wa kuendelea kutoa huku wadau wengine wakiendelea kuhamasika kuunga mkono juhudi za serikali kwa kuchangia miradi ya maendeleo.

Awali uongozi wa halmashauri ya Arusha, kwa kushirikiana na Mwenyekiti wa halmashauri, Baraza la waheshimiwa Madiwani na watalamu, wanawakaribisha wadau wa maendeleo kujitikeza kwa wingi kuendelea kuchangia miradi mbalimbali ya halmashauri ya Arusha.


ARUSHA DC TUPO TAYARI KUHESABIWA ✍
SHIRIKI SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022
JIANDAE KUHESABIWA 23.08.2022


PICHA ZA MATUKIO WAKATI WA KUKABIDHI  VYETI VYA PONGEZI


Diwani wa kata ya Sokon II, Mhe. Obedi Mollel (kushoto) kipokea cheti cha shukurani kwa kuchangia mapokezi ya Mwenge wa Uhuru 2022, kutoka kwa Mwenyekiti wa halmashauri ya Arusha Mhe,. Ojung'u Salekwa wakati wa mkutano wa Baraza la madiwani kwenye ukumbi wa mikutano halmashauri ya Arusha. 



Mchungaji Philemon Olais Mollel (kushoto) kipokea cheti cha shukurani kwa kuchangia mapokezi ya Mwenge wa Uhuru 2022, kutoka kwa Mwenyekiti wa halmashauri ya Arusha Mhe,. Ojung'u Salekwa wakati wa mkutano wa Baraza la madiwani kwenye ukumbi wa mikutano halmashauri ya Arusha.


Mkurugenzi wa shirika la Walking in Love (kushoto) kipokea cheti cha shukurani kwa kuchangia mapokezi ya Mwenge wa Uhuru 2022, kutoka kwa Mwenyekiti wa halmashauri ya Arusha Mhe,. Ojung'u Salekwa wakati wa mkutano wa Baraza la madiwani kwenye ukumbi wa mikutano halmashauri ya Arusha.



Mwakilishi wa shirika la CWCD (kushoto) kipokea cheti cha shukurani kwa kuchangia mapokezi ya Mwenge wa Uhuru 2022, kutoka kwa Mwenyekiti wa halmashauri ya Arusha Mhe,. Ojung'u Salekwa wakati wa mkutano wa Baraza la madiwani kwenye ukumbi wa mikutano halmashauri ya Arusha.


Mchungaji Philemon Olais Mollel (kushoto) kipokea cheti cha shukurani kwa kuchangia mapokezi ya Mwenge wa Uhuru 2022, kutoka kwa Mwenyekiti wa halmashauri ya Arusha Mhe,. Ojung'u Salekwa wakati wa mkutano wa Baraza la madiwani kwenye ukumbi wa mikutano halmashauri ya Arusha.


Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.