Na.Elinipa Lupembe
Mkurugenzi Mtendaji, halmashauri ya Arusha Seleman Msumi, amewataka watumishi wa Umma kushiriki michezo, kwa kuwa michezo inafaida nyingi kiafya, inajenga mahusiano mazuri ikiwa ni pamoja ushirikiano, umoja, upendo, katika maeneo ya kazi.
Mkurugenzi Msumi ameyasema hayo wakati wa maandalizi ya mchezo wa kirafiki kati ya timu za watumishi wa halmashauri ya Arusha na timu ya watumishi wa Halmashauri ya Meru zote za wilaya ya Arumeru, mashindano yaliyofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita, kwenye viwanja vya Viwanja vya Ngarenaro Complex vya Jijini Arusha.
Mkurugenzi huyo ameeleza umuhimu wa michezo kwa watumishi wa umma, kuwa ni pamoja na kuimarisha afya zao, kujenga upendo na ushirikiano baina yao, pamoja na kuondoa msongo wa mawazo unaotokana na kazi nyingi, zinazosababisha watumishi kutumia muda mwingi kutekeleza majukumu yao ya kikazi.
"Watumishi mnapaswa kufahamu, michezo huimarisha utendaji kazi, michezo ni afya, michezo ni furaha, amani na upendo, baada ya kutekeleza majukumu ya kazi, niwatake watumishi wote kujitokeza kushiriki michezo, jambo ambalo litamfanya mfanyakazi 'kurelax' na kuondoa msongo wa mawazo pamoja na kujiimarisha katika utekelezaji bora wa majukumu yake ya kikazi" amesisitiza Mkurugenzi huyo.
Aidha, mkurugenzi huyo amewahimiza wachezaji wa timu ya halmashauri yake ya Arusha, kuiwakilisha vema halmashauri hiyo, kucheza kwa umakini na kutumia mbinu zote walizofundishwa na walimu wao, ili kuzipatia tiimu zao ushindi dhidi ya wapinzani wao wa halmashauri ya Meru.
Hata hivyo baada ya mashindano hayo kufanyika, kwa matokeao ya jumla halmashauri ya Arusha, ilibuka kidedea dhidi ya wapinzani wao wa halmashauri ya Meru.
Afisa Michezo halmashauri ya Arusha, Priscus Silayo, amethibitisha kiwa, timu ya halmashauri ya Arusha, kufanya vema katika michuano hiyo, huku akiweka wazi matokeo ya michezo iliyofanyika kuwa ni pamoja na mpira wa miguu, ambapo timu ya Arusha Dc na Meru Dc zilitoka sare kwa kufungana goli 2-2, wakati mpira wa Pete matokeo yalikwa sare kwa kufungana magoli 8-8, huku mpira wa Wavu, timu ya Arusha Dc ikiibuka kidedea kushindi wa seti 2 kwa sufuri na kuwalaza mahasimu wao wa Meru DC.
Arusha DC hatujawahi kushindwa
Win#win#
#kaziiendelee# ✍✍
PICHA ZA MATUKIO
Picha ya pamoja, Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha, Seleman Msumi ( mwenye truck suit nyekundu) na wachezaji wa timu ya watumishi wa halmashauri ya Arusha, muda mfupi kabla ya kuanza mchezo wa kirafiki dhidi ya timu ya watumishi wa halmashauri ya Meru, michezo iliyofanyika kwenye viwanja vya Ngarenaro Complex vya Jijini Arusha.
Picha ya pamoja, Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha, Seleman Msumi ( mwenye truck suit nyekundu) na wachezaji wa timu ya Mpira wa Pete, halmashauri ya Arusha, muda mfupi kabla ya kuanza mchezo wa kirafiki dhidi ya timu ya watumishi wa halmashauri ya Meru, michezo iliyofanyika kwenye viwanja vya Ngarenaro Complex vya Jijini Arusha.
Picha ya pamoja, Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha, Seleman Msumi ( mwenye truck suit nyekundu) na wachezaji wa timu ya Mpira wa Miguu, halmashauri ya Arusha, muda mfupi kabla ya kuanza mchezo wa kirafiki dhidi ya timu ya watumishi wa halmashauri ya Meru, michezo iliyofanyika kwenye viwanja vya Ngarenaro Complex vya Jijini Arusha.
Picha ya pamoja, Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha, Seleman Msumi ( mwenye truck suit nyekundu) na wachezaji wa timu ya Mpira wa Wavu, halmashauri ya Arusha, muda mfupi kabla ya kuanza mchezo wa kirafiki dhidi ya timu ya watumishi wa halmashauri ya Meru, michezo iliyofanyika kwenye viwanja vya Ngarenaro Complex vya Jijini Arusha.
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.