Na Elinipa Lupembe
Jumla ya wanamichezo 120 wamechaguliwa kuiwakilisha halmashauri ya Arusha kwenye mashindano ya wanafunzi wa shule za sekondari - UMISETA ngazi ya mkoa, baada ya kukamilisha mashindano ya ngazi ya halmashauri mapema jana.
Akizungumza wakati wa kuhitimisha mashindano hayo ngazi ya halmashauri, yaliyofanyika kwenye viwanja vya shule ya sekondari Ilboru, Mkurugenzi mtendaji, halmashauri ya Arusha Seleman Msumi, amewapongeza wanamishezo hao waliochaguliwa na kuwataka kwenda kuipeperusha vema bendera ya halmashauri hiyo.
Aidha amewapa wachezaji hao siri ya mafanikio ni kujiandaa vizuri, kusikiliza na kufuata maelekezo ya makocha wao, pamoja ma kuwa na nidhamu wakati wote wa mashindano.
"Nidhamu ni nguzo imara ya mafanikio, unaweza kuwa mchezaji mzuri lakini ukiwa huna nidhamu ni sawa na bure, ninawaomba vijana wangu, tuongozwe na nidhamu, iwakilisheni vema halmashauri na Taifa" Amesema Mkurugenzi Msumi
Naye Mkuu wa Idara ya Elimu sekondari, Halmashauri ya Arusha Mwl. Menard Lupenza, kundi lililochaguliwa ni kundi bora sana, kupitia vipaji mlivyonavyo mkiongeza na maelekezo ya makocha wenu ili kufikia malengo ya ushindi, huku mkitambua kuwa michezo nia ajira.
Licha ya kuwashukuru walimu kwa kujitoa kuandaa wanafunzi tangu ngazi ya shule, amewataka kuendelea kuwasimamia mpaka ngazi ya Taifa na kuhakikisha wanarudi na ushindi kama ilivyokuwa mwaka jana wa 2022.
Michezo shuleni licha ya kuwa ni afya, zaidi inainua vipaji nje ya taaluma, mizcheao ni utekelezaji wa KPI program ya kuondoa mdondoko shuleni, inayowafanya wanafunzi kupenda kuhudhuria shule". Amebainisha Mwl. Lupenza
Afisa Michezo,halmashauri ya Arusha Priscus Silayo, amesema kuwa wanafunzi hao 120, wamechaguliwa kati ya wanafunzi 840 walioshiriki michezo ya fani za ndani na nje kwa ngazi ya halmashauri, kutoka shule za sekondari, ikijumuisha michezo ya aina 7, ikiwemeo soka, netiboli, mpira wa wavu, kikapu, mikono, riadha na fani za ndani.
"Tumeshindanisha timu za shule kutoka kanda tano za Ilboru, Mringa, Mlangarini, Kisongo na Ngaramtoni kwa kushirikiaha walimu kwa kuzingatia vigezo na uwezo wa kujituma katika michezo, pamoja na nidhamu.
Kaulimbiu ya UMISEMTA 2023: Uimarishaji wa miundombinu nchini ni chachu ya Maendeleo ya Taaluma, Sanaa na Michezo nchini
ARUSHA DC ni Yetu, Tushirikiane Kuijenga"
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.