Na Elinipa Lupembe
Wajumbe wa Kamati ya fedha Utawala na Mipango, halmashauri ya Arusha, wakikagua mradi wa Kiwanda cha Kufyatua matofali eneo la Mlangarini, mradi unaomilikiwa na halmashauri hiyo.
Kuanzishwa kwa Mradi huo kumegharimu kiasi cha shilingi milioni 30, kwa fedha za Mapato ya Ndani na umeanza rasmi utekelezaji wake, ikiwa ni mradi kwa ajili ya mapato ya ndani.
Ziara hiyo ya kikazi ya kamati ya Fedha, Utawala na Mipango ni ya kawaida kwa mujibu wa Sheria na Kanuni za uendeshaji wa serikali za Mitaa kwa kuzingatia Utawala Bora wa uwazi na uwajibikaji.
Halmashauri ya Arusha inawakaribisha wananchi wote, kununua matofali kwenye kiwanda hicho cha Umma.
ARUSHA DC
KaziIendelee✍✍
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.