Wajumbe wa Kamati ya Siasa CCM wilaya ya Arumeru wakikagua Mwenyekiti wakikagua mradi wa ujenzi wa nyumba ya mwalimu shule ya msingi Olemedeye kata ya Laroi, mradi uliotekelezwa kwa gharama ya shilingi milioni 50 fedha kutoka Serikali Kuu.
Wajumbe hao wameridhishwa na utekelezaji wa mradi huo, ambao kutekelezwa na umekamilika kwa wakati, ukithibitisha ubora na thamani ya fedha zilizotumika (value for money) na tayari walimu wataanza kuishi hapo.
Mwenyekiti CCM Wilaya hiyo, Noel Severe, amepongeza hali ya utekelezaji wa mradi huo, na kuipongeza serikali ya awamu ya sita namna inavyotekeleza Ilani ya CCM ya mwaka 2020 -2025 kwa vitendo.
Akisoma taarifa ya mradi huo, Afisa Mtendaji kata ya Laroi, ameweka wazi kuwa, Mradi ulianza kutekelezwa mwezi Septemba 2022,kwa kutumia force account, na tayari umekamilika kwa 100% na walimu wanategemea kuanza kuishi hapo.
Naye Diwani wa kata ya Laroi na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Arusha, Mhe. Dkt. Ojung'u Salekwa, licha ya kuishukuru serikali kwa mradi huo wa nyumba za walimu, ameelezea changamoto za kutembea umbali mrefu walizokuwa wakipata walimu kufika shuleni hapo.
Amefafanua kuwa mradi huo, utawawezesha walimu kuishi ndani ya eneo la shule na kuepuka kutembea umbali wa zaidi ya Kilomita 15 kutoka eneo ambalo kuna nyumba za kupangisha huku akiamini kupanda kwa taaluma shuleni hapo.
Ziara hiyo ni maalumu kwa ajili ya ufuatiliaji wa utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi ya mwaka 2020 - 2025.
"Arusha DC ni Yetu, Tushirikiane Kuijenga"
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.