• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

MAAFISA WATENDAJI KATA 8 ARUSHA DC, WAPATA MGAO WA  PIKIPIKI ZA SERIKALI.

Posted on: February 18th, 2023

Na Elinipa Lupembe

Maafisa watendaji wa kata 8 halmashauri ya Arusha  wamekabidhiwa pikipiki zilizotolewa na serikali kwa lengo la kuboresha utendaji kazi na kurahisisha utoaji wa huduma kwa wananchi nchini.

Akizungumza wakati wa hafla fupi ya kukabidhi pikipiki hizo, Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha, Seleman Msumi amesema kuwa pikipiki hizo ni vifaa muhimu kwa Maafisa hao zinazokwenda kumaliza changamoto ya kutembea umbali mrefu kuwafikia wanachi ili kutoa huduma.

Ameweka wazi kuwa, kata hizo 8 ziko maeneo ya pembezoni zikiwa na maeneo makubwa ya kiutendaji hivyo Maafisa hulazimika kutembea muda mrefu kuwafikia wananchi kutoa huduma jambo ambalo linakwenda kumalizika sasa.

Aidha amewataka Maafisa hao kutumia pikipiki hizo kwa ajili ya kazi iliyokusudiwa na serikali ya kuwahudumia wananchi na si vinginevyo huku akiwasisitiza kuzitunza na kuzithamini kwa kutambua kuwa ni mali ya Umma.

"Tunamshukuru Mhe. Rais kwa kuwatahamini Maafisa Watendaji wa kata, kwa kuwa wao ndio wanawahudumia wananchi moja kwa moja, Watendaji mnalo deni sasa,  mkatumie vifaa hivi kulingana na malengo yaliyokusudiwa na si kwa matumizi binafsi". Amesisitiza Mkurugenzi Msumi

Naye Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi wilaya ya kichama Arumeru, Komredi Noel Severe, ameipongeza serikali kwa kuteketeleza Ilani ya Chama hicho kwa vitendo, kwa kuhakikisha watumishi wanapata vitendea kazi vitakavyorahisisha utoaji na upatikanaji wa huduma kwa wananchi katika maeneo yao.

"Serikali inawategemea, mmepata usafiri, tumieni muda mwingi kutatua kero na changamoto za wananchi kwenye maeneo ya vijiji na vitongoji vyenu kwa wakati, kwa kufanya hivyo, tutafikia malengo ya serikali ambayo ndio maagizo ya Ilani". Amesisitiza Mwenyekiti huyo wa CCM

Hata hivyo Maafisa Watendaji hao, wameipongeza serikali ya awamu ya sita, inayoongozwa na Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuona umuhimu wa kuwapatia usafiri, jambo ambalo wamekiri lilikiwa ni changamoto kubwa iliyokwamisha utendaji kazi katika maeneo yao.

Afisa Mtendaji wa kata ya Oldonyosambu, Lomnyaki Ndiyogi licha ya kuipongeza serikali amekiri changamoto ya kutembea umbali mrefu wa takribani Kilomita hamsini, jambo lililowafanya kutumia zaidi ya masaa nane kufanya kazi moja.

"Kupitia pikipiki hizi zinakwenda kuongeza ufanisi katika utendaji kazi wetu, jambo la kufanya siku nzima sasa tutatumia saa moja, tunamshukuru Mama Samia na tunaahidi kuwahudumia wananchi kwa kasi kubwa sasa". amefafanua Lomnyaki.

Halmashauri ya Arusha ni miongoni mwa halmashauri nchini iliyopata pikipiki 8 kati ya pikipiki 916 zilizotolewa na serikali na kuzigawa kwa Maafisa wa kata za pembezoni za Bwawani Oljoro, Laroi, Musa, Oldonyowas, Oldonyosambu  Lemanyata na Sambasha.


Arusha DC

KaziInaendelea✍✍


PICHA ZA MATUKIO WAKATI WA MAKABIDHIANO YA PIKIPIKI








Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • DKT. PASCAL KATIKA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA

    June 19, 2025
  • WIKI YA UTUMISHI WA UMMA

    June 18, 2025
  • MAADHIMISHO YA WIKI YA UTUMISHI

    June 17, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.