Na Elinipa Lupembe.
Mbunge wa Jimbo la Arumeru Magharibi, Mhe. Noah Lembris, amewasistiza viongozi wawakilishi wa wananchi wakiwemo waheshimiwa madiwani, wenyeviti wa vijiji na vitongoji halmashauri ya Arusha kuendelea kushiriki kuhamasisha utekelezaji wa zoezi la Sensa ya Watu na Makazi, itakayofanyika nchini tarehe 23.08.2022.
Mhe. Noa ametoa rai hiyo wakati wa mkutano wa Baraza la Madiwa la robo ya nne na ya mwisho kwa mwaka wa 2021/2022 kwa kiwasisistiza viongozi hao, kushiriki kuhamasisha wananchi katika maeneo yao kushiriki Sensa ya Watu na makazi na kuhakikisha kila mtu aliyelala kwenye mipaka ya eneo lake usiku wa kuamkia siku ya Sensa anahesabiwa.
Amesema kuwa zoezi la Sensa ni muhimu kwa maendeleo ya nchi yetu, lakini pia ni muhimu kwa maendleeo ya kata na vijiji vyetu, ikiwa ni mkakati wa mipango thabiti ya kuwahudumia wananchi kulingana na idadi yao kwenye eneo husika.
"Madiwani na wenyeviti wa vijiji na vitongoji mnajukumu la kuwaelimisha na kuwahamasisha wananchi wenu umuhimu wa kuhesabiwa siku hiyo ya Sensa, sambamba na kuhakikisha watu wote waliolala kwenye eneo lako usiku wa kuamkia siku ya Sensa wanahesabiwa bila kukosa" Amesisitiza Mbunge Noah.
Naye Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha, Seleman Msumi, amebainisha kuwa tofauti na Sensa zilizopita, Sensa ya watu na makazi 2022, imenasibishwa kuwa ni Sensa shirikishi, ambayo viongozi wote wenye dhamana wanalojukumu la kushiriki katika zoezi hilo muhimu kwa kuhakikisha watu wote katika maeneo yao wanahesabiwa siku ya Sensa.
Naye Mratibu wa Sena Halmashauri ya Arusha Innocent Matick, ameeleza kuwa kwa mujibu wa muongozo wa sensa ya watu na makazi Madiwani ni wenyeviti wa kamati ya Sensa ngazi ya kata hivyo wanawajibu wa kuhamasisha sensa katika kata zao kwa kuhakikishao zoezi linafanyika kwa uafilifu huku watu wote katika maenwo yao wanahesabiwa.
Ameongeza kuwa, kadhalika wenyeviti wa vijiji na vitongoji ndio wenyeviti wa kamati ya Sensa ngazi ya vijiji na vitongoji, wakiwa na jukumu kubwa la kuhakikisha kila mtu aliyelala kwenye eneo lake usiku wa kuamkia siku ya sensa anahesabiwa kwa kutoa taarifa kwa karani wa sensa kupitia dodoso la sensa.
Sensa ya watu na makazi inatarajiwa kufanyika tarehe 23.08.2022 nchini, ikiwa na kengo la kukusanya taarifa za wananchi na maifa sahihi za Kidemografia, Kijamii, Kiuchumi na Mazingira, takwimu sahihi zitakazoiwezesha Serikali na wadau wengine kupanga mipango ya maendeleo kisekta.
ARUSHA DC TUPO TAYARI KUHESABIWA✍
MHE. NOAH YUPO TAYARI KUHESABIWA✍
SHIRIKI SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022
JIANDAE KUHESABIWA 23.08.2022✍
SENSABIKAAAAAAAA
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.