Na Elinipa Lupembe
Katika kutekelazaji wa mikakati ya serikali ya kuboresha miundo mbinu kwenye vituo vya kutolea huduma za Afya, serikali imefanikiwa kuwekeza kwenye ujenzi wa nyumba za watumishi lengo likiwani kuhakikisha wananchi wanapata huduma za afya katika maeneo yao na kwa muda wote.
Katika mwaka wa fedha 2021/2022, halmashauri ya Arusha ilipokea kiasi cha shilingi milioni 200 fedha kutoka Serikali kuu kwa ajili ya ujenzi wa nyumba 4 za watumishi kwenye vituo 4 vya Afya vilivyopo maeneo ya pembezoni.
Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha Seleman Msumi, amebainisha kuwa kiasi hicho cha fedha kimetumika kujenga nyumba 4 za watumishi wa afya kwa gharama ya shilingi milioni 50 kwa kila nyumba.
"Fedha hizo zimejenga nyumba za watumishi kwenye maeneo ambayo watumishi hawakuwa na mahali pa kuishi na kulazimika kuishi mbali na vituo vyao vya kazi, nyumba hizi zimejengwa kwenye zahanati za LoovLukuny na Ilkerini kata ya Kisongo, zahanati ya Ilkirevi kata ya Oltoroto, na kituo cha Afya Nduruma".Amefafanua Mkurugenzi Msumi
Naye Mkuu wa Idara ya Mipango, Anna Urio, amesema kuwa fedha hizo ni utekelezaji wa malengo ya bajeti ya halmashauri ya mwaka wa fedha 2021/2022 ulioishia June 2022 wa kuboresha mazingira ya watumishi ili kuongeza tija na ufanisi katika kazi.
Naye Mganga Mfawidhi zahanati ya Ilkirevi kata ya Olturoto, Atu Sanga, amsema kuwa uwepo wa nyumba ya mtumishi wa afya, utaongeza tija na ufanisi wa kazi, ikiwa nipamoja na kutoa huduma za afya kwa masaa 24.
"Mtumishi akiishi eneo la kazi inampunguzia gharama za kulipa kodi ya nyumba lakini inatuwezesha kutoa hudma za emergence hasa nyakati za usiku, wagonjwa wanakuwa na uhakika wa kupata matibabu". Amefafanua Mganga huyo Mfawaidhi.
Hata hivyo Diwani wa kata ya Olturoto, ameishukuru seikali ya awamu ya sita chini ya uongozi wa Mheshimwa Samia Suluhu Hassan, kwa utekelezaji wa Ilani ya CCM, katika sekta zote hususani sekta ya afya, sekta ambayo ni muhimu kwa afya za wananchi.
"Ninampongeza na kumshukuru mheshimiwa Rais, kwa niaba ya wananchi wa Olturoto, ujenzi wa nyumba ya mtumishi ni wazi utaongeza tija katika utendaji wa kazi lakini uwanda mpana wa upatikanaji na utoaji wa huduma za afya kwa wananchi sambamba na kupunguza vifo vya wanawake na watoto" Amesisitiza Mhe. Simon
Ujenzi wa miundombinu ya afya ni utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2020 -2025 wa kuongezeka vituo kutolea huduma za afya nchini ikiwemo zahanati, vituo vya afya na hospitali pamoja na nyumba za wahudumu wa afya.
ARUSHA DC
KaziInaendelea ✍✍✍
PICHA ZA MAJENGO YA NYUMBA ZA WATUMISHI
Muonekano wa Nyumba ya Mtumishi Kituo chaAfya Nduruma kata ya Nduruma
Muonekano wa Nyumba ya Mtumishi Zahanati ya Loovilukuny kata ya Kisongo
Muonekano wa Nyumba ya Mtumishi Zahanati ya Ilkerini kata ya Kisongo
Muonekano wa Nyumba ya Mtumishi Zahanati ya Ilkerini kata ya Kisongo
Muonekano wa Nyumba ya Mtumishi Zahanati ya Ilkirevi kata ya Olturoto
Muonekano wa Nyumba ya Mtumishi Zahanati ya Ilkirevi kata ya Olturoto
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.