Na Elinipa Lupembe
Mvua kubwa iliyonyesha usiku wa kuamkia tarehe 23.03.2023 imesababisha uharibufu mkubwa kwa wananchi wa maeneo ya Ngaramtoni.
Jumla ya kata tano za Oloirien, Olmotonyi, Olturumet, Kimnyaki na Kiranyi zimeathirika na matokeo ya mvua hiyo kubwa ambayo haikusababisha maafa kwa binadamu.
Mvua hiyo imeharibu miundombinu ya barabara, kuvunja kuta za baadhi ya nyumba, mifereji kujaa tope, kuharibu mashamba huku maji na matope yakijaa ndani ya nyumba na kuharibu samani za ndani kwa baadhi ya nyumba.
Mkuu wa wilaya ya Arumeru, Mhe. Emanuela Mtatifikolo Kaganda, anatoa pole kwa wananchi wote kutokana na uharibifu na hasara zote zilizosababishwa na mvua hiyo na kuwataka wananchi kuendelea kuchukua tahadhari ya mvua zinazoendelea kunyesha katika msimu huu wa mvua.
Aidha amewashukuru wakazi wa maeneo hayo, ndugu jamaa na marafi kwa kuwawapa misaada mbalimbali ya kibinadamu wale walioathirika zaidi, na kusisitiza udugu huo uendelee kuwepo katika maisha yetu ya kila siku.
"Ninashukuru kwa kuwa wananchi wote waliungana kukabiliana na majanga yaliyotokea kwa kuwasaidia wale walioathithika zaidi, huu ndio upendo ambao Mwenyenzi Mungu ameusisitiza katika maisha yetu wanadamu". Amesisitiza Mhe. Emanuela
ARUMERU
#kaziinaendela✍✍✍
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.