Na. Elinipa Lupembe.
Mwanamke wa kwanza kufanyiwa upasuaji, kwenye kituo cha Afya Nduruma, mara baada ya kituo hicho kujengwa majengo mapya ikiwemo jengo la upasuaji, ametoa ushuhuda wa furaha aliyonayo, mbele ya Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mhandusi Joseph Mwamhanga, wakati wa ziara yake ya kikazi ndani ya halmashauri ya Arusha.
Mwanamke huyo aliyejitambulisha kwa jina la Maria Seleman, amesema kuwa, wakati wa ujauzito wake alipanga kujifungulia kwenye kituo hicho cha afya, mara baada ya serikali kujenga kuboresha miundo mbinu ya kituo hicho, na awali hakufahamu kuwa angetakiwa kujifungua kwa njia ya upasuaji.
Baada ya kufikishwa katika kituo hicho cha afya na kufanyiwa uchunguzi na madaktari, walishauri kufanyiwa upasuaji na kumfanya kuwa mgonjwa wa kwanza kutumia jengo hilo jipya la upasuaji, huku akiwashukuru wahudumu wa afya kwa huduma bora waliompatia, mpaka sasa wanaendelea vizuri yeye na mtoto wake wakiwa wenye nguvu na afya bora.
Hata hivyo, katibu mkuu huyo, a mefurahishwa na ushuhuda wa mama huyo, aliyepata huduma ya upasuaji katika kituo hicho cha afya na kusisitiza kuwa hilo ndio lengo la Serikali ya awamu ya tano, la kupunguza vifo vya mama na mtoto wakati wa kujifungua kwa kujenga vituo vya afya na kuboresha huduma hizo, ili kuhakikisha wananchi wote wanapata huduma ndani ya maeneo yao bila kutembea umbali mrefu.
Aidha amewataka wananchi wa eneo hilo kuthamini gharama zilizotumika kuwekeza kwenye majengo na vifaa tiba, na kufahamu kuwa kituo hicho ni mali yao na kuwahimiza kukitunza na kukilinda, huku akiwataka wauguzi na madaktari kutoahuduma stahiki kwa wagonjwa bila ubaguzi.
Aidha Katibu mkuu, ameahidi kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa jengo la Mionzi 'X-ray' katika kituo hicho, kwa kuwa tayari serikali imeshaleta vifaa vya mionzi, na kumuagiza mkurugenzi wa halmashauri, kufanza makisio ya gharama za ujenzi wa jengo hilo.
"Kwa kuwa tayari vifaa vya x-ray vimeshafika, niahidi kutafuta fedha za kujenga jengo la mionzi kwa haraka ili vifaa hivyo vianze kutumika na wananchi wapate huduma zote kituoni hapo" amesema Katibu mkuu huyo.
Naye mkuu wa wilaya ya Arumeru, Jerry Muro, licha ya kuishukuru na kuipongeza serikali ya Rais Magufuli, ameahidi kuendelea kusimamia utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi ndani ya wilaya yake, kwa kuhakikisga wananchi wanapata huma bora kwa sekta zote, kama mikakati ya serikali inavyoelekeza.
Akisoma taarifa ya kituo hicho, Mganga Mfawidhi wa Kituo cha afya Nduruma Dkt. Joseph Ideva, amesema kuwa serikali ilitoa kiasi cha shilingi milioni 500 kwa ajili ya ujenzi wa jengo la mama na mtoto, jengo la upasuaji, maabara, jengo la kuhifadhia maiti, kichomea taka, nyumba ya mganga, pamoja na kuleta vifaa tiba vyenye thamani ya shilingi milioni 327 ambapo majengo yote yamekamilika na tayari wananchi wameanza kupata huduma.
Ameongeza kuwampaka sasa upatikanaji wa dawa za msingi, katika kituo hicho ni wa zaidi ya asilimia 95, na kuwataka wananchi kufika kituoni hapo kupata huduma za afya na kuachana na dhana potofu za kwenda kwenye hospitali za binafsi.
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.