Na. Elinipa Lupembe.
Mwili wa alieyekuwa Katibu Tawala mkoa wa Arusha, marehemu Richard Kwitega umewasili, kwenye uwanja wa ndege wa Mwanza, kwa ndege ya shirika la ndege Tanzania - Air Tanzania na kupokelewa na mkuu wa mkoa wa Mwanza, mheshimiwa John Mongela.
Mwili wa huo, umewasili uwanjani hapo majira ya saa 10:20 jioni, ukitokea mkoani Arusha, ukiongozwa na Mkuu wa mkoa wa Arusha, mheshimiwa Idd Kimanta akiwa ameambatana na viongozi wengine wa chama na serikali, kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa, watumishi wa mkoa wa Arusha pamoja na familia ya mareheu Kwitega mke na watoto.
Mwili wa marehemu Kwitega, umeelekea kwenye makazi yake ya Mwanza, mtaa wa Ikigiju, kata ya Nyamongolo Manispaa ya Ilemela, kwa ajli ya maombelezo na kuagwa na wakazi wa mkoa wa Mwanza, na baadaye kesho kuelekea nyumbani kwao, katika kijiji cha Ngoma wilayani Sengerema kwa ajili ya mazishi.
Maremu Richard Kwitega, amefariki dunia siku ya Jumatano tarehe 03.02.2021 saa tisa alasiri, kwa ajili ya gari iliyotokea eneo la Mdolii-Babati mkoani Manyara akiwa njiani kuelekea Dofoma kikazi.
Mwenyenzi Mungu ailaze roho ya marehemu mahala pema peponi. Amina.
PICHA ZA MATUKIO MWANZA AIR PORT
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.