TANGAZO TANGAZO TANGAZONAFASI ZA WANAFUNZI WA KUJIUNGA NA SHULE YA MSINGI Mhe. MAMA SAMIA ACADEMY.
Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Arusha, Seleman Msumi, anawatangazia Wazazi na Walezi wenye watoto waliofikisha umri wa kuandikishwa Darasa la Awali na Darasa la Kwanza kuleta watoto hao, kuandikishwa kwenye shule mpya ya Msingi ya Mchepuo wa Kiingereza kwa mwaka wa masomo unaonza Januari 2022.
Shule ya Msingi Mhe. MAMA SAMIA ACADEMY ni shule ya Serikali inayomilikiwa na Halmashauri ya Arusha,Shule ya MAMA SAMIA ACADEMY inapokea pia wanafunzi wa kuhamia kwa darsa la 2, 3 na la 4.Shule ni ya kutwa, ipo kata ya Mlangarini eneo la Chekereni, karibu na Ofisi ya Kata Mlangarini, mlete mwanao afundishwe na walimu wenye uwezo na uzoefu wa kulea watoto Kimwili, Kiakili, Kiroho na Kijamii.Ada zetu ni nafuu, na unaweza kulipa kwa awamu.
Fomu za Kujiunga zinapatikana shule ya Msingi Olomitu eneo la Chekereni kwa gharama ya Tsh. 10,000/=
Kwa mawasilano Zaidi piga simu Na. 0784 954 554
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.