Na Elinipa Lupembe.
Jumla ya mashirika yasiyo ya kiserikali 30 kati ya 46 ya yanayofanyakazi ndani ya mipaka ya halmashauri ya Arusha, wilaya ya Arumeru, yamewasilisha taarifa za robo ya nne kwa mwaka 2022, huku mashirika hayo yakisisitizwa kuelimisha jamii juu ya ulawiti kwa watoto wa kiume.
Mashirika hayo yamewasilisha taarifa zao zilizoainisha utekelezaji wa shughuli za maendeleo zilizofanywa na mashirika hayo kwa kipindi cha robo hiyo ya nne na ya mwisho kwa mwaka 2022, kwenye mkutano uliofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa halmashauri ya Arusha.
Katika kikao hicho kila mwakilishi wa shirika alipata wasaa wa kuelezea utekelezaji wa shughuli na miradi ya maendeleo iliyofanyika kwa kipindi cha robo hiyo huku wakielezea ongezeko la matukio ya ulawiti yanayowakabili watoto wa kiume ndani ya jamii kwa sasa.
"Kama mashirika tunapswa tuone namna ya kuelekeza nguvu za kuhamasisha na kutoa elimu kwa watoto wa kiume kujitambua na kujilinda dhidi ya ulawiti, huku tukihamasisha jamii kuwalinda watoto wa kiume kama ilivyo kwa watoto wa kike.
Aidha Mashirika hayo yamepongeza utaratibu huo unaofanywa na serikali na kuueleze ni utaratibu unaowakutanisha pamoja na kufahamiana huku kila shirika likifahamu miradi innayofanywa na shirika jingine katika eneo husika.
Amesema kuwa uwepo wa kikao hicho licha ya kufahamiana, unawapa fursa ya kubadilishana uzoefu na kuwajengea uwezo namna ya kutatua changamoto zinazoikabili jamii
Hata hivyo mkurugenzi mtendaji halmashauri ya Arusha Seleman Msumi, ameweka wazi kuridhishwa na shughuli zinazofanywa na ASAS hizo katika halmashauri, miradi ambayo inawakwamua wananchi kutoka kwenye hali duni na kwenda hali nzuri.
Ameongeza serikali inatambua na kuthamini kazi zinazofanywa na ASAS za kiraia, kwa kuwa mnaisaidia serikali kutimiza majukumu yake ya kuihudumia jamii.
"Serikali inaendelea kuweka mazingira rafiki kwa mashirika kwa kutambua umuhimu wa huduma mnazozitoa kwa jamii, ni huduma za kiimani zaidi, mngeweza kufanya vinginevyo lakini mmejikita kuwahudumia wananchi hususani wasio na uwezo ili wajikwamue". Amefafanua Msumi.
Naye mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii halmashauri ya Arusha Stedvant Kileo, ameyataka mashirikia hayo kuona namna ya kuwekeza nguvu katika kuwalinda na kuwajengea uwezo watoto wa kiume dhidi ya vitendo vya ulawiti, matukio ambayo yameshika kasi katika jamii yetu.
"Niwaombe mashirika katika miradi mnayoifanya, kuingiza agenda ya kupinga na kupambana na matukio ya ulawiti kwa watoto wa kiume, changamoto ambayo inashika kasi kwenye jamii kwa sasa". Amesisitiza Kileo
Kikao hicho kimefanyika kwa mujibu wa sheria za serikali zinayoyataka mashirika yasiyo ya kiserikali kuwasilisha taarifa za utekelezaji wa shughuli na miradi wanayoifanya kila robo ya mwaka, mwaka unaoanzia mwezi Januari mpaka Desemba.
"ARUSHA DC ni Yetu, Tushirikiane Kuijenga"
#KaziIendelee✍✍
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.