• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

SELEMAN MSUMI DED ARUSHA DC AANZA HIVI: CHEO NI DHAMANA, WATUMISHI TUNA DHAMANA YA KUWATUMIKIA WANANCHI

Posted on: August 9th, 2021

Na. Elinipa Lupembe.

Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha, Seleman Msumi, ameikumbusha timu ya Menejimenti halmashauri hiyo, kutambua kuwa cheo ni dhamana, hivyo watumishi wanapaswa kutumia dhamana hiyo kwa kuwatumikia wananchi wa halmashauri ya Arusha.

Mkurugenzi Msumi, ameyasema hayo, alipokutana kwa mara ya kwanza na timu ya menejimenti ya halmashauri ya Arusha, kwenye kikao mkakati cha wiki mamarufu kama 'morning prayer' ambapo alitumia nafasi hiyo kujitambulisha, timu  inayojumuisha wakuu wa Idara na Vitengo, na kuwataka kufanya kazi kwa bidii kwa lengo la kuwatumikia wananchi, kwa maendeleo ya halmashauri na taifa kwa ujumla.

Aidha Mkurugenzi Msumi, ameweka wazi kuwa, anazo taarifa kuwa halmashauri ya Arusha, ni moja kati ya halmashauri nchini zinazofanya vizuri katika sekta zote, na kufuatia matokeo mazuri yaliyofanywa na watangulizi wake, yuko tayari kuyaendeleza kwa kushirikiana na watumishi wote wa halmashauri ya Arusha, kufanya kazi kama timu na kila mmoja kutumia ujuzi alionao kufuatia maekelekezo ya kazi kwa kada husika, huku wakizingatia kanuni, sheria, taratibu na miongozo ili kufikia malengo yaliyowekwa. 

"Ninaamini kwenye kufanya kazi kwa ushirikiano, kwa pamoja kama timu, mimi ni muumini wa 'team work', mkurugenzi hawezi kufikia malengo kama wakuu wa Idara, wakuu wa vitengo na watumishi wengine hawata nia mamoja, ninachotamani kila mtu awe active, aheshimu wengine, afanye kazi kwa uaminifu na kwa moyo wa uzalendo bila kusukumwa wala kusimamiwa kwa karibu, kwa kuwa kila mtu ana mpango kazi wake na ana malengo yatakayopimwa kwenye mpango kazi huo". Amefafanua Mkurugenzi Msumi.

Mkurugenzi Msumi, licha ya kuwapongeza na kuwashukuru watumishi wa halmashauri hiyo kwa kumpokea, ameweka wazi hisia na matamanio yake, kuwa anatamani watumishi siku moja halmashauri ya Arusha kuwa halmashauri namba moja nchini inayoongoza kisekta katika masuala ya ukusanyaji mapato, elimu afya na maji na maendeleo kwa ujumla.

Hata hivyo, mkurugezi huyo, amewataka viongozi hao kuwa mstari wa mbele katika kupambana na UVIKO 19, kwa kuhamasisha jamii, kufuata maelekezo yanayotolewa na watalamu wa afya ikiwemo, kunawa mikono kwa sabuni na maji tiririka, kuvaa barakoa, tumia vitakasa mikono pamaoja na kuepuka misongamano.

Naye Afisa Elimu Msingi, mwalimu Hossein Mghewa, aliyekaimu kiti hicho cha ukurugenzi, amemkaribisha mkurugezi Msumi na kumponhez kwa kuteuliwa kwake, kuiongoz halamshauri ya Arusha pamoja  na kumuahidi kumpa ushirikiano, kwa kufanya kazi kwa bidii ili kufikia maono ya halmashauri kwa kuifanya kuwa halmashauri inayoongoza kwa kutoa huduma bora kwa jamii na maendeleo endelevu ifikapo 2025.

Mkurungenzi Msumi, aliyeteliwa tarehe 01.Augosti, 2021 na  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan,  kuwa Mkurugenzi Mtendaji, halmashauri ya Arusha, anakuwa ni mkurugenzi wa sita kuongoza halmashauri ya Arusha, tangu ilipogawanywa iliyokuwa halmashauri ya wilaya ya Arumeru Julai 1, 2007 na kupata halamshauri ya Arusha na Meru, zote zikiwa wilaya ya Arumeru.


Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha, Seleman Msumi, akizungumza kwa mara ya kwanza na timu ya Menejimenti inayojumuisha Wakuu wa Idara na Vitengo, kwenye kikao kazi cha wiki maarufu kama 'Morning Parayer', kwenye ukumbi wa mikutano wa halmashauri hiyo.









Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • DKT. PASCAL KATIKA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA

    June 19, 2025
  • WIKI YA UTUMISHI WA UMMA

    June 18, 2025
  • MAADHIMISHO YA WIKI YA UTUMISHI

    June 17, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.