TAARIFA KWA UMMA/VYOMBO VYA HABARI.
Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha Seleman Msumi, anautaarifu Umma kuwa Halmashauri imepokea fedha kiasi cha shilingi Milioni 115.6 kwa awamu mbili kutoka Serikali Kuu kupitia miradi ya GPE - LANES II kwa ajili ya kutekeleza miradi ya ujenzi wa miundombinu ya shule mbili za Msingi.
Mkurugenzi Msumi amefafanua kuwa kiasi hicho cha fedha kitatumika kujenga miundombinu ya madarasa ya awali ya mfano kwa shule mbili, ikiwemo shule ya Msingi Ngorbob kata ya Matevesi na shule ya Msingi Olokii kata ya Bwawani.
Aidha kila shule itajengwa vyumba viwili vya madarasa na samani zake, michezo ya watoto (bembea), matundu sita ya vyoo huku matundu mawili ya vyoo yakiwa ni maalum kwa Wanafunzi wenye Mahitaji Maalum kwa shule zote mbili.
Mkurugenzi Msumi amefafanua lengo la Serikali kutoa fedha hizo ni kuboresha miundombinu ya shule za awali nchini kwa kujenga shule za awali za mfano zenye vifaa vyote muhimu (Nursery Model School), ili kukuza stadi za Kusoma, Kuandika na Kuhesabu kwa wanafunzi wa shule za msingi.
Mchanganuo wa fedha hizo na Miradi itakayotekelezwa imeainishwa kwenye jedwali:-
NA.
|
JINA LA MRADI |
KATA |
KIASI CHA FEDHA |
|
SHULE YA MSINGI NGORBOB
|
MATEVES |
57,824,000.00 |
|
SHULE YA MSINGI OLOKII
|
BWAWANI |
57,825,000.00 |
JUMLA |
115,649,000.00 |
Elinipa J. Lupembe
KAIMU MKUU WA KITENDO CHA MAWASILIANO SERIKALINI
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.