• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

SHIRIKA LA CWCD LAZINDUA PROGRAM YA KUPAMBANA NA UKATILI WA WATOTO, KIPINDI HIKI CHA CORONA

Posted on: May 30th, 2020

Na. Elinipa Lupembe.

Shirika lisilo la kiserikali la Center for Women, Children and Youth Development la Arusha, limeanzisha programu maalumu ya kutoa elimu ya ukatili kwa watoto, katika kipindi hiki cha mlipuko wa ugonjwa wa homa kali ya Mapafu inayosababishwa na virusi vya COVID 19, kwenye kata za halmashauri ya Arusha, wilaya ya Arumeru.

Imeelezwa kuwa programu hiyo maaluu, itatekelezwa  kwenye kata 17 kwa kuwashirikisha Maafisa Watendaji wa kata, waendesha Bodaboda, watoa huduma za afya ngazi ya jamii na watalamu wa halmashauri ya Arusha kisekta, lengo likiwa kuelimisha jamii kupambana na ukatili dhidi ya watoto katika kipindi hichi ambacho jamii iko kwenye taharuki ya kukabiliana na ugonjwa wa Corona.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa programu hiyo maalumu, iliyoambatana na mafunzo kwa watalam hao,Mratibu wa Mradi shirika la CWCD Fatuma Ally, amesema kwamba, uanzishwaji wa programu hiyo, umekuja  baada ya kuripotiwa kwa vitendo vya ukatili dhidi ya watoto, vinavyoendelea kwenye jamii, wakati jamii imejikita kwenye kupambana na ugonjwa wa Corona.

Fatuma ameeleza kuwa, katika kipindi hiki cha likizo maalumu kwa ajili ya Corona, kipindi ambacho watoto wako nyumbani, imeripotiwa kuna baadhi ya watoto wa kike wamepata ujauzito, wengine wakiozwa na wengine wamekuwa wakiingiliana kimwili ndani ya familia moja, hivyo ni vema kutoa elimu kwa jamii ya kuzuia ukatili huo wakati wakikabiliana na gonjwa la Corona.

"Tumeshuhudia matukio ya ukatili kwenye vyombo vya habari,  huko Tunduru karibia watoto 100 wamepata ujauzito, lakini familia nyingine mzazi anaomba ushauri mtoto wa kiume amewapa mimba dada zake, shirika limeona njia pekee ni kutoa elimu kwa jamii, ili kuondokana na tatizo hilo "amesema Mratibu huyo wa Miradi CWCD.

Naye Afisa Maendeleo ya Jamii, halmashauri ya Arusha, Angela Mvaa, amethibitisha kuripotiwa kwa matukio ya ukatili dhidi ya watoto ikiwa ni pamoja na watoto kuolewa, visa ambavyo vimetokea kipindi hiki ambacho serikali, ilichukua hatua ya kuzifunga shule ili kuzuia maambukizi ya ugonjwa wa Corona.

Amewataka Maafisa Watendaji wa kata hao, kufuatilia watoto walioko nyumbani, kama wako salama na endapo kuna watoto wamefanyiwa ukatili watoe taarifa haraka, kwa kuwa tayari kuna fununu ya baadhi ya wazazi wameanza kuwaozesha watoto wa kike.

"Serikali inafahamu idadi ya watoto waliokuwa shuleni, hivyo Watendaji wa kata pitieni maeneo yenu, kuhakikisha watoto wote wako salama na watarudi wote shuleni, endapo kuna mtoto, hatapatikana toeni taarifa ili hatua zichukuliwe" amefafanua Afisa huyo.

Aidha Maafisa Watendahi wa kata hizo, licha ya kushukuru kwa mradi huo, wamekiri kuwa na changamoto za ufuatiliaji wa kesi za ukatili dhidi ya watoto, ikielezwa kuwa upelelezi unaendelea na hatimaye kesi kuisha kiholela.

Afisa Mtendaji kata ya Kisongo, Brighton Mwanri, amethibitisha kuwa, amekwishapeleka kesi tatu tofauti kwenye kituo cha polisi, na kesi hizo kupotelea huko, huku watuhumiwa wakiachiwa huru na kupoteza haki za watoto.

Hata hivyo wakati wa mafunzo ya program hayo, shirika la CWCD liligawa vifaa vya kujikinga na maambukizi ya ugonjwa wa Corona kwa ajili ya kutumika kwenye Ofisi za Kata hizo,na jumla ya ndoo 17 za kunawia mikono  pamoja na dawa kinga za kuulia vijidudu, wakati wa kunawa mikono.

Programu hii ya muda mfupi inatekelezwa na halmashauri ya Arusha na shirika la CWCD kwa ufadhili wa shirika la  Foundation for Civil Society  la nchini Tanzania na itafanyika kwa kijpindi cha miezi mitatu kuanzia sasa.







Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.