• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Shule zaagizwa kuanzisha Dawati la kupokea malalamiko ya matukio ya ukatili dhidi ya watoto

Posted on: June 17th, 2018

Na. Elinipa Lupembe.

Serikali kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Watoto na wazee, imezitaka shule zote Tanzania, kuanzisha Dawati maalumu la malalamiko ambalo watoto watapata fursa ya kutoa taarifa za ukatili watakaofanyiwa kwenye jamii zao. 

Agizo hilo limetolewa na Mkurugenzi Msaidizi Idara ya watoto, Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Watoto na Wazee, Sebastian Kitiku, wakati wa mdahalo wa wanafunzi wa shule ya msingi Engalaoni kata Mwandeti, halmashauri ya Arusha, uliofanyika shuleni hapo.

Kitiku amesema kuwa, Dawati hilo maalumu, litajihusisha na kupokea malalamiko ya watoto wanaofanyiwa matukio ya ukatili na kuyashughulikia huku itoa fursa kwa watoto, kuchagua walimu watatu kwenye shule zao, walimu ambao, watoto wenyewe wataona ni walimu rafiki na wao watakua huru kuwaeleza hali yoyote ya ukatili au viashiria vya ukatili utakaofanyika dhidi yao.  

Aidha Kitiku amefafanua kuwa, Dawati hilo ni mkakati endelevu wa Wizara, utakaoongeza mtandao wa watoto kutoa taarifa ya matukio ya ukatili katika kuendeleza na kurahisisha, mapambano dhidi ya ukatili wanaofanyiwa watoto.  

Aidha ameongeza kuwa licha ya dawati hilo,  Wizara imeongeza njia za kutoa taarifa kupitia simu ya bure kwa kupiga namba 116 na kutoa taarifa muda wowote.

 "Namba 116 itatumika kutoa taarifa ya ukatili dhidi ya mtoto, mtoto mwenyewe anaruhusiwa kipiga simu na mtu yoyote atatumia namba hiyo kutoa taarifa za ukatili wa mtoto kwa muda wowote atakapokuwa ana taarifa yoyote ile". Amesema Kitiku.

Aidha, Wakati wa mdahalo huo, watoto wa shule ya msingi Engalaon, walionesha kusikitishwa na mila na desturi za jamii yao ya Kimaasai za kuwaozesha watoto wa kike wakiwa na umri mdogo huku wakilazimika kukatishwa masomo na ndoto zao za maisha.

Watoto hao wameongeza kuwa mila za kimasai, licha ya kandamizi kwa wanawake na watoto wa kike lakini pia upo ukatili kwa watoto wa kiume ambao huwazuia kwenda shule na badala yake kuachwa nyumbani wakichunga ng'ombe.

Hata hivyo watoto hao wamethibitisha wao wenyewe kuanza, kupambana na mila hizo kandamizi, kupitia klabu iliyoanzishwa shuleni hapo mwaka jana na shirika la WDCD baada ya kugundulika kuwa zaidi ya wasichana 70 shuleni hapo walikuwa wamechumbiwa, wakisubiri kuolewa.

Aidha watoto hao wamesema kuwa kupitia klabu hiyo, wamepata elimu juu ya haki zao na namna ya kukabiliana na mila hizo huku wakitoa taarifa pale wanapofanyiwa vitendo vya ukatili.

Naio Baraka mmoja wa wanafunzi aliyekuwa amechumbiwa, amesema kuwa baada ya kujifunza haki zake kupitia klabu ya watoto shuleni hapo, na taryari alikuwa amechumbiwa, aliweza kutoa taarifa kwa uongozi wa kijiji na shule na baadae baba yake kulazimika kurudisha mahari, na sasa yupo shule anaendelea na masomo, akiwa mwenye matumaini makubwa ya kutimiza ndoto yake ya kuwa mwalimu.

"Baba yangu alitaka kuzima ndoto yangu ya kuwa mwalimu, kwa kutaka kuniozesha kwa mwaname mzee, nikiwa na miaka 14, ninafurahi amerudisha mahari, sasa nitakuwa mwalimu na kuelimisha jamii". Amesema Naio.

Hata hivyo uongozi wa kijiji cha Engalaoni, unaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali kutoa elimu kwa jamii hiyo, kuachana na mila potofu huku jamii hiyo ikiendelea kubadilika.

Mwenyekiti wa Kamati ya shule ya msingi Engalaoni, Mzee Laizer amethibitisha kuwa kwa sasa jamii imeanza kuelimika na kutaka serikali kuwaelimisha taratibu kwa kuwa hizo ni mila ambazo walirithi kwa mababu zao, na hapo awali, hawakufahamu madhara yake.

"Jamii yetu haikufahamu kuwa mila hizi zina madhara makubwa kwa watoto, na sisi tumezirithi kutoka kwa mababu na mababu, hivyo naomba serikali iendelee kutuelimisha tuu, na wengi wameanza kuelewa sasa" amesema Laizer.

Hata hivyo, licha ya mapambano dhidi ya ukatili wa watoto, tafiti zinaonyesha bado hali ni mbaya, watoto wakike 3 kati ya 10 wanafanyiwa ukatili huku mtoto 1 wa kiume kati ya 10 anafanyiwa ukatili wa kingono, na asilimia 49 ya matukio hayo hufanyika nyumbani na ndugu wa familia, asilimia 23 hufanyika njiani na asilimia 15 hufanyika shuleni.

Mdahalo huo umefanyika kwa lengo la kusikiliza changamoto za watoto wakati wa kuelekea maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika mkoa wa Arusha, yatakayofanyika  tarehe 13.06.2018 kwenye viwanja vya sheik Amri Abeid, Jijini Arusha yenye Kauli mbiu ya 'KUELEKEA UCHUMI WA VIWANJA, TUSIMUACHE MTOTO NYUMA'.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.