TAARIFA KWA UMMA/VYOMBO VYA HABARI.
MATUMIZI YA FEDHA SHILINGI MILIONI 85.4 ZA MAPATO YA NDANI KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI SITA SEKTA YA ELIMU NA AFYA.
Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha Seleman Msumi, anautaarifu Umma kuwa Halmashauri imetenga fedha kiasi cha shilingi Milioni 85.4 fedha za Mapato yake ya Ndani kwa ajili ya kutekeleza miradi 6 ya Maendeleo katika sekta ya Elimu na Afya, kwa kipindi cha robo ya nne ya mwaka wa fedha 2022/2023.
Aidha Mkurugenzi Msumi ameitaja miradi hiyo kuwa ni pamoja na ukamilishaji wa vyumba vya madarasa jengo la ghorofa (ground floor) shule ya sekondari Ilkiding’a, ukamilishaji wa vyumba viwili ya madarasa shule ya Msingi Shibolo, ujenzi wa matundu 8 ya vyoo shule ya Msingi Olomitu na ujenzi wa matundu 6 ya vyoo shule ya sekondari Nduruma.
Miradi mingine ni ukamilishaji wa zahanati ya Kigongoni, ujenzi wa nyumba ya mtumishi Zahanati ya Bwawani, usimikaji wa mfumo wa kukusanyia mapato (GoTHOMIS) zahanati ya Bangata na Oldadai.
Mchanganuo wa fedha hizo na Miradi itakayotekelezwa imeainishwa kwenye jedwali:-
NA.
|
JINA LA MRADI |
SHUGHULI ZITAKAZOFANYIKA |
KIASI CHA FEDHA |
|
SHULE YA SEKONDARI ILKIDING’A
|
Ukamilishaji wa vyumba vya madarasa ghorofa ya kwanza |
20,000,000.00 |
|
SHULE YA MSINGI SHIBOLO
|
Ukamilishaji wa vyumba 2 vya madarasa |
10,000,000.00 |
|
SHULE YA MSINGI OLOMITU
|
Ujenzi wa matundu 8 vya vyoo |
8,800,000.00 |
|
SHULE YA SEKONDARI NDURUMA
|
Ujenzi wa matundu 6 vya vyoo |
6,600,000.00 |
|
ZAHANATI YA KIGONGONI
|
Ukamilishaji wa Zahanati |
10,000,000.00 |
|
NYUMBA YA MTUMISHI
|
Ukamilishaji wa nyumba ya mtumishi Zahanati ya Bwawani |
10,000,000.00 |
|
ZAHANATI YA OLDADAI
|
Ufungaji wa Mfumo wa Kukusanyia Mapato (GoTHOMIS) |
10,000,000.00 |
|
ZAHANATI YA BANGATA
|
Ufungaji wa Mfumo wa Kukusanyia Mapato (GoTHOMIS) |
10,000,000.00 |
JUMLA |
|
85,400,000.00 |
Elinipa Lupembe
KAIMU MKUU WA KITENDO CHA MAWASILIANO SERIKALINI (W)
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.