• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

TASAF YAONDOA CHANGAMOTO YA KIVUKO KITONGOJI CHA MOIVO.

Posted on: July 13th, 2022

Na Elinipa Lupembe

Serikali kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii - TASAF imetekeleza mradi wa ujenzi wa kivuko kitongoji cha Moivo kata ya Moivo halmashauri ya Arusha, changamoto ambayo ilihatarisha maisha ya watu na mali zao wa eneo hilo.

Wakizungumza mara baada ya Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha, Seleman Msumi, kuzindua  Kivuko hicho, wananchi wa Moivo licha ya kuishukuru TASAF kwa kuwajengea kivuko, wameeleza madhara yaliyowapata kabla ya kuwa na kivuko ni pamoja na watu kuporwa mali zao na vibaka, wanawake kubakwa huku wengine wakinusurika kuuawa na watoto kushindwa kwenda shule hasa wakati wa mvua kwa kushindwa kupita hapo.

Eliamani Shange ambaye ni mnufaika wa TASAF, ameweka wazi  kuwa, kuwepo kwa kivuko hicho sasa kumeondoa kero zote hizo, hakuna tena kichaka cha  vibaka hapo na kubwa zaidi sasa watoto wanakwenda shule kwa amani, huku kivuko hicho kikitarajiwa kukuza uchumi wa eneo hilo kwa kuwa wafanya biashara wanasafirisha bidhaa zao kwa urahisi tofauti na hapo mwanzo.

"Hiki kivuko kimetusaidia sana kina mama na watoto, lakini pia  kimewarahisishia wajasiriamali kusafirisha bidhaa zao, kama unavyoona magari sasa yanapita hapa yamebeba bidhaa mbalimbali, zamani watu tulibeba kichwani, tunaishukuru sana TASAF ni mkombozi wa jamii na mali zao, usafiri ni wa uhakika usiku na mchana" amesisitiza Mwajabu Hassan

Naye Diwani wa kata ya Moivo Mhe.  Selina Mollel, ameipongeza serikali kupitia TASAF kwa kuwaondolea wananchi wake kero ya muda mrefu,  sambamba na kuwapongeza walengwa wa TASAF kwa kujenga kivuko hicho kwa mikono yao kupitia mpango wa ajira za muda unaowawezesha walengwa kufanya kazi katika miradi hiyo

"Kipekee niwapongeze walengwa wa TASAF, mmefanya kazi kubwa na nzuri, mmesimama imara na kuhakikisha kivuko kimepatikana kama lilivyokuwa hitaji lenu la muda mrefu, mmefanya kazi kwa moyo bila kukata tamaa, hadi ujenzi umekamilika, serikali yetu inahitaji wananchi wazalendo kama ninyi"  Amesisitiza Mhe. Selina.

Hata hivyo Mkurugenzi Mtendaji, halmashauri ya Arusha, Seleman Msumi, amewataka wananchi hao wa Moivo, kukitunza kivuko hicho ili kidumu na kuwaletea mabadiliko ya kijamii na kiuchumi, kwa kuwa tayari serikali imetimiza jukumu lake la kuwawekea miundombinu hiyo kazi yao ni kutumia na kutunza na kusisitiza kuwa mama Samia ameupiga mwingi.

"Kuwepo kwa kivuko katika eneo hili, ni chanzo cha maendeleo katikaneneo hili, kitarahisisha kusafirisha mazao, kuasafirisha bidhaa kwa wafanayabiashara na hata suala la wagonjwa litakuwa rahisi, ambulance zitafika sasa hadi nyumbani" amesisitiza Msuimi

Awali mradi wa Kivuko cha Moivo, umetekelezwa na TASAF kupitia programu za ujenzi wa miundombinu na Ajira za muda, kwa gharama ya shilingi milioni 68 huku asilimia 50 ya fedha hizo zikitumika kununua vifaa na asilimia 50 ikitumika kulipa ujira kwa wanufaika wa mpango wa kunusuru kaya masikini kwa lengo la kuwaongezea kipato.


ARUSHA DC

KaziInaendelea✍

JIANDAE KUHESABIWA


PICHA ZA MATUKIO WAKATI WA UZINDUZI WA KIVUKO CHA MOIVO.



Kutoka kushoto, Mwenyekiti wa usimamizi wa ujenzi CMC, Brazard Mkwizu, Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha Seleman Msumi (katikati) na Diwani kata ya Moivo Mhe. Selina Mollel, wakikata utepe kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa ujenzi wa kivuko cha Moivo, Mradi uliotekelezwa na TASAF III awamu ya II



Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha Seleman Msumi akizungumza na wananchi wa Moivo wakati wa uzinduzi wa mradi wa ujenzi wa kivuko cha Moivo, Mradi uliotekelezwa na TASAF III awamu ya II


Mwenyekiti wa kamati ya ujenzi wa kivuko - CMC   Brazard Mkwizu, akisoma taarifa ya mradi wa ujenzi wa kivuko cha Moivo


Mwonekano wa kivuko cha Moivo mara baada ya kukamilika, na tayati kimeanza kutumika














Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.