Na. Elinipa Lupembe.
Ubalozi wa Japan nchini Tanzania, umeridhishwa na uyekelezaji wa mradi wa ujenzi wa vyumba vya madarasa shule ya sekondari Sokon II, halmashauri ya Arusha, wilayani Arumeru.
Akizungumza na mwandishi wetu, Mratibu wa Miradi kutoka Ubalozi wa Japan, nchini Tanzania, Ayumi Kasai, alipotembelea na kukagua mradi huo, amethibitisha kuridhishwa na kasi ya utekelezaji wa ujenzi wa vyumba vya madarasa, mradi unaofadhiliwa na Ubalozi wa Japani nchini.
Ayumi amesema kuwa, licha ya kuwa ujenzi huo, umeanza mwezi Mei 2019, mpaka sasa umeekamilika kwa zaidi ya asilimia 55 jambo ambalo linatia moyo na kuleta matumaini ya kukamilika kwa wakati kulingana na mkataba wa ujenzi.
Hata hivyo Ayumi ameupongeza uongozi wa halmashauri ya Arusha kwa ujumla wake, kwa usimamizi imara wa miradi na kuongeza kuwa, kutokana na ushirikiano wa Ubalozi wa Japani na halmashauri ya Arusha, Ubalozi huo umejipanga kuendelea kutekeleza mradi mwingine ndani ya halmashauri hiyo.
Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji, Afisa Elimu Taaluma, halmashauri ya Arusha, John Charles, amesema kuwa, halmashauri inathamini mchango mkubwa unaotolewa na Ubalozi wa Japani, hasa katika sekta ya Elimu, sekta ambayo ni nyeti kwa manufaa ya Taifa la Tanzania na vizazi vyake.
Ameongeza kuwa, halmashsuri itahakikisha mradi huo, unakamilika kwa wakati, na madarasa hayo kuanza kutumika, madarasa ambayo yanategemewa kupunguza, msongamano wa wanafunzi unaosababishwa na uhaba wa vyumba vya madarasa uliopo shuleni hapo kwa sasa.
"Nikuhakikishie kuwa, ujenzi huu utakamilika kwa wakati, na wanafunzi wataanza kuyatumia ndani ya mwaka huu, na kupunguza msongamano wa wanafunzi uliopo kwa sasa" amesema Charles.
Naye mkuu wa shule ya Sekondari Sokon II, mwalimu Mwamvita Kilonzo, amesema kuwa, vyumba hivyo vya madarasa vitachukua jumla ya wanafunzi 180 kwa uwiano wa wanafunzi 45 kwa darasa moja.
Ameongeza kuwa, shule ya Sokoni II ina vyumba 11 vya madarasa ikiwa na uhitaji wa vyumba 11 zaidi, ikiwa na jumla ya wanafunzi 993, na kuongeza kuwa kukamilika kwa vyumba hivyo vinne, vitaongeza idadi na kubakiza upingufu wa vyumba saba.
Ubalozi wa Japani nchini Tanzania, umetoa fedha kiadi cha shilingi milioni 195, kwa ajili ya ujenzi wa msingi wa ghorofa na ukamilishaji wa vyumba vinne vya madarasa, vyoo vya wanafunzi pamoja na samani za madarasa yote, mradi ulionza kutekelezwa mwezi Mwei 2019 na unategemea kukamilika mapema ifikapo mwezi wa Oktoba 2019.
Mratibu na msimamizi wa Miradi, Ubalozi wa Japani, Ayumi Kasai, akikagua ramani ya Jengo la ghorofa vyumba vinne vya madarasa shule ya sekondari Sokon II, kulia ni Mhandisi wa Idara ya Ujenzi, Mhandisi Bibie Manzi.
Mratibu na msimamizi wa Miradi, Ubalozi wa Japani akikagua ujenzi wa Jengo la ghorofa vyumba vinne vya madarasa shule ya sekondari Sokon II.
Muonekano wa Jengo la ghorofa vyumba vinne vya madarasa shule ya sekondari Sokon II.
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.