Na. Elinipa Lupembe.
Utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa vyumba 100 vya madarasa halmashauri ya Arusha umeanza kwa kasi, ukiwa katika hatua za awali kutegemea na maeneo, huku asilimia kubwa wakiwa kwenye hatua ya msingi na maeneo mengine wakiwa wameanza kupandisha kuta.
Utekelezaji wa mradi huo mkubwa wa ujenzi wa vyumba 100 vya madarasa kujengwa kwa wakati mmoja, mradi ambao haujawahi kufanyika, tangu kuanzishwa kwa halmashauri ya Arusha, unatekelezwa kufuatia fedha za mgao wa kutoka serikalini kuu, kwa ajaili ya mapambano dhidi ya UVIKO 19.
Naye Kurugenzi Mtendaji, halmasahuri ya Arusha, Seleman Msumi, amesema kuwa ujenzi huo umeanza kwa kasi, katika shule zilizopokea fedha hizo, ukitumia mfumo wa 'force akaunti', na kuahidi kusimamia utekeleza wa mradi huo kwa weledi, ili uweze kukamilika kwa wakati na kwa viwango vinavyoendana na thamani ya fedha, kama ilivyo agizo la serikali la kukamilisha mradi huo kabla ya tarehe 15, Desemba 2021.
Naye Afisa Elimu sekondari, halmashauri ya Arusha, Mwalimu Menard Lupenza, ameutaja mgao huo wa vyumba 100 vya madarasa katika halmashauri hiyo, kuwa jumla ya vyumba 96, vinajengwa kwenye shule zote 30 za sekondari za serikali, huku shule 2 za msingi shikizi zikijengwa vyumba 4 vya madarasa, mradi unaogharimu kiasi cha shilingi bilioni 2, ikiwa na mgawanyo wa shilingi milioni 20 kwa kila darasa.
"Mgao huo wa idadi ya vyumba vya madarasa, umezingatia upungufu wa vyumba vya madarasa uliokuwepo, kwa ulinganifu wa idadi ya wanafunzi katika shule husika, huku shule ya sekondari Kiranyi ikipata idadi kubwa kuliko shule zote, ikiwa na jumla ya vyumba 13, ikifuatiwa na shule ya sekondari Ilkiding'a, vyumba 11 na shule ya sekondari Mringa ikijengwa vyumba 10". ameweka wazi Afisa Elimu huyo.
Mkuu wa shule ya sekondari Mringa, Mwalim Salum Magaka, amesema kuwa, shule hiyo inatekeleza mradi wa ujenzi wa vyumba 10 vya madarasa kwa gharama ya shilingi milioni 200, fedha za mapambano dhidi ya UVIKO 19 na kuongeza kuwa ujenzi wa vyumba hivyo vyote uko kwenye hatua ya msingi na unategemewa kukamilisha kwa wakati na kwa ubora.
"Tunaamini tutakamilisha mradi huu kwa wakati, kwa kuwa tayari tumeshanunua vifaa vyote vya muhimu vinavyohitajika, tumepokea 'materials' yote, kazi iliyobaki hapa ni usimamizi, kumsimamia fundi kwa kuzingatia hatua zote za ujenzi, ili kukamilisha madarasa yote 10, kwa wakati na kwa ubora unaoendana na thamani ya fedha" amesisitiza mkuu huyo wa shule.
Awali halmashauri ya Arusha, imepata mgao wa shilingi bilioni 2 kutoka shilingi trillioni 1.3 za mkopo wenye riba nafuu kutoka Shirika la Fedha Duniani - IMF, ikiwa ni fedha za Mpango wa Maendeleo kwa Ustawi wa Taifa na Mapambano dhidi ya UVIKO 19, kwa ajili ya ujenzi wa vyumba 96 vya madarasa shule za sekondari na Vyumba 4 vya madarasa shule 2 shikizi za Msingi.
ARUSHA DC
KaziInaendelea✍✍
PICHA ZA HATUA MBALIMBALI ZA UJENZI.
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.