• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WAATHIRIKA WA VVU WASHAURIWA KUACHANA NA IMANI POTOFU BADALA YAKE KUENDELEA KUTUMIA ARAV

Posted on: May 10th, 2022

Na.Elinipa Lupembe.

Waathirika wa virusi ya UKIMWI, wameshauriwa kuachana na imani potofu, zinazowasababisha kuacha, kutumia dawa za kufubaza virusi vya UKIMWI - ARV. Rai hiyo imetolewa na wakati wa mkutano wa Baraza la Madiwani Halmashauri ya Arusha, wa robo ya tatu mwaka wa fedha 2021/2022, mkutano uliofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa halmasahuri hiyo.

Akizungumza wakati wa kipindi cha maswali ya papo kwa papo, Diwani wa Kata ya Kimnyaki Mhe. Eliakimu Marivey,  ameuliza nini mkakati wa halmashauti kwa watu wanoishi na virusi vya UKIMWI, na kuamua kuacha kutumia dawa za kufubaza virusi hivyo, kutokana na imani potofu zinazotokana na mila na desturi.

Akijibu swali hilo, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Arusha, Selemani Msumi ameweka wazi kuwa, serikali kupitia watalamu wa sekta zote, inaendelea kutoa elimu kwa jamii, juu ya umuhimu wa vidonge vya kufubaza makali ya Virusi vya UKIMWI, na kuwataka viongozi wa mila na wale wa dini kutoa elimu sahihi kwa waumini wao kuhusu matumizi ya dawa hizo.

“Mara nyingi watu wamekuwa wakisitisha matumizi ya Dawa za Magonjwa kama Pressure na UKIMWI kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kuchoshwa na dawa hizo pamoja na imani potofu, badala yake wanatumia dawa za miti shamba, hali inayopelekea kufupisha Maisha yao, niwaombe viongozi wenzangu tushirikiane kuelemisha jamii katika maeneo yetu”. Amesema Msumi.

Hata hivyo baadhi ya wajumbe waliohudhuria katika kikao hicho cha Madiwani, wamesema kuwa wataendelea kushirikiana na serikali kutoa elimu kwa jamii na kuifanya agenda ya kudumu kwenye mikutano ya vijiji, lengo likiwa ni kuwaelisha jamii matumizi sahihi ya dawa za ARVs pamoja na umuhimu wa dawa hizo kwa maisha.

“Ninawashauri watu wenye maambukizi waendelee kutumia Dawa za kufubaza Virusi Vya Ukimwi kwasababu kuacha kutumia dawa hizo ni kuhatarisha maisha ya mtu binafsi, pia na wale watakaobainika kutoa elimu isiyo sahihi serikali iwachukulie hatua za kisheria”. Amesema Mhe. Elinipa Laizer, Diwani Viti Maalum

Mkutano huo wa Baraza la Madiwani umejikita kujadili utekelezaji wa shughuli za halmashauri, ikiwemo utekelezaji wa miradi ya maendeleo kiseta, mapato na matumizi pamoja na shughuli za maendeleo ya jamii na  ustawi wa jamii zilizotekelezwa katika maeneo yote ndani ya Halmashauri katika kipindi cha robo ya tatu ya kuanzia mwezi Januari hadi Machi 2022.

ARUAHA DC

KaziIendelee✍✍





Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.