• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WAKULIMA ARUSHA DC WAANZA KUNUFAIKA NA PROGRAMU YA ANZIA SOKONI MALIZIA SHAMBANI KWA KIPATO ZAIDI....

Posted on: May 28th, 2023

Na Elinipa Lupembe


Wakulima wanaojishughulisha na kilimo cha mbogamboga halmashauri ya Arusha, wameanza kunufaika na programu ya Anzia Sokoni Malizia Shambani kwa Kipato zaidi, mradi unayotekelezwa na shirika la TANSHEP kwa ufadhili wa JICA.

Wakulima hao wamethibitisha hayo, walipotembelewa na mwandishi wetu kwanye mashamba yao  katika kata za Bangata na Shambasha na kujionea hali halisi ya kilimo biashara kinachofanywa na wakulima hao.

Neema  Mathayo, mkulima mbogamboga kijiji cha Midawe kata ya Bangata amesema kuwa walipata mafunzo ya kufanya tafiti za kuanzia sokoni kutafiti bei za mazao kwa msimu husika kabla ya kuamua kulima zao flani, ndipo hali ya kilimo ilipoanza kubadilika kwa na kuwa kilimo biashara kwa uhalisia wake.

"Hapa tumelima viazi, kwa kufanya tafiti wa soko kabla ya kulima, pindi tutakapovuna uhitaji wa viazi utakuwa mkubwa na bei yake itakuwa kubwa pia, kwa kuwa tumelenga msimu mzuri kwa soko" Amesema Neema

Mzee Joel Labarani, ameweka wazi kuwa programu ya anzia sokoni, imewafanya wakulima kulima kilimo cha kisasa kinachoendana na mahitaji ya soko, na kuwaondoa kwenye kilimo cha mazoea cha kulima tuu ilimradi umeotesha mazao shambani.

Naye Dina Erasto mkulima kwa kata ya Sambasha, amesema kuwa progamu ya anzia sokoni malizia shambani, imeanza kuwaondoa madalali wa mazao ambao waliwanyonya kwa muda mefu, na kuongeza kuwa wakulima sasa wanayomawasiliano ya moja kwa moja na wafanyabiashara sokoni, hivyo mkulima anaamua kumuzia dalali ama kwenda sokoni moja kwa moja kwa kuzingatia bei halisi ya soko.

Hata hivyo Ester Michael,  ameishukuru serikali kupitia watalamu wa kilimo ngazi ya kata na halmashauri ya Arusha  kwa kuwa na wakulima bega kwa bega, kuwapa ushauri wa kitaalamu pamoja na kuwaunganisha na wadau wengine wa kilimo, masoko na ujasiriamali, unaowawezesha wakulima kuendelea kufanya kilimo biashara.

Awali Mkuu wa Kitengo cha Kilimo, halmashauri ya Arusha, Bahati Mtweve, amesema kuwa programu hiyo ya anzia sokoni malizia shambani kwa kipato zaidi ni utekelezaji wa mkakati wa serikali wa Agenda 10, 30 ya kilimo biashara.

"Kwa sasa wakulima wameanza kunufaika na kilimo, kwanza kwa kulima zao kulingana na mahitaji ya soko  na pia kuuza mazao yao kwa kuzingatia bei ya soko bila kunyonywa na wachuuzi ambao walinufaika sana na jasho la mkulima". Amefafanua Afisa Kilimo Bahati

Halmashauri ya Arusha kupitia Idara ya Kilimo kwa kushirikiana na wadau wa kilimo wanaendelea kutoa mafunzo ya utalamu wa  kilimo kwa wakulima husasani kilimo cha kisasa kitakachowaletea kipato zaidi na kufikia Agenda 10/30 ya Kilimo Biashara.

"ARUSHA DCNi Yetu, Tushirikiane Kuijenga"
#KaziIendelee





Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.