• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WAMATA YAWAONDOLEA KERO YA MAJI WANAWAKE WA THEMIYASIMBA

Posted on: September 25th, 2022

Na Elinipa Lupembe.

Shirika lisilo la kiserikali la WAMATA limewaondolea kero ya maji ya muda mrefu, iliyokuwa ikiwakabili wanawake wa kitongoji cha Nyamagana kijiji cha Themiyasimba kata ya Bwawani, sio tu kwa matumizi ya nyumbani bali kwenye zahanati ya Themiyasimba kwa kina mama wakati wa kujifungua.

Shirika hilo limefanikiwa kujenga mradi wa maji kwa kuchimba kisima kirefu, kuweka matanki ya kuhifadhiamaji pamoja vituo vya kuchotea maji kwa gharama ya shilingi milioni 100, mradi utakaowawezesha wakazi wa kitongoji cha hicho na majirani, shule na zahanati kupata maji safi na salama jambo ambalo halijawahi kutokea kijijini hapo.

Wananchi wa kitongoji hicho, wamelishukuru shirika hilo na kuelezea hisia zao, wakati wa uzinduzi wa mradi huo, namna wanawake walivyokuwa wanateseka kupata maji kwa matumizi ya familia lakini zaidi kwenye zahanati ambayo kina mama wajawazito walikuwa wanakosa maji hasa wakati wa kujifungua.

Happy Kaaya, mkazi wa Nyamagana, amesema kuwa, adha ya maji katika kitongoji hicho iliwapotezea wanawake muda mwingi wa kutembea umbali wa zaidi ya Kilometa 5 kutafuta maji, jambo ambalo lilidhoofisha hali ya afya na uchumi wa familia zao.

"Sisi wanawake tumepata mkombozi, sisi ndio tulikuwa wahanga wakubwa wa ukosefu wa maji, tulitumia muda mrefu kutafuta maji, lakini zaidi tunafuraha pale ambapo maji yamefika kwenye zahanati yetu ya Themiyasimba, hivyo kinamama hatutateseka tena wakati wa kujifungua" Ameweka wazi Happy

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mradi huo wa maji, Mkurugenzi wa shirika la WAMATA, John Tarimo amesema kuwa shirika hilo kwa ufadhili wa shirika la World Server la nchini Marekani, limefanikisha mradi huo wa maji, mara baada ya kuona adha kubwa ya maji iliyokuwa inawakabili wananchi wa Bwawani hususani kijiji cha Themiyasimba.

 Hata hivyo, Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Arusha amewashukuru wadau wa shirika hilo kwa kutoa huduma hiyo muhimu kwa wananchi wa Themiyasimba, ikiwa ni utekelezaji wa malengo ya Serikali ya awamu ya sita ya kumtua mama ndoo.

"Serikali inathamini kazi zinazofanywa na wadau za kufanikisha vipaumbele vya Serikali, WAMATA mmewezesha kumtua mama ndoo ikiwa ni sera ya Serikali ya awamu ya sita, inayoongozwa na mama Samia Suluhu Hassan". Amesisitiza Mkurugenzi Msumi

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa kijiji cha Themiyasimba, Mhel Mussa Msengi, ameshukuru kwa mradi huo wa maji, kwa kuwa changamoto ya maji ilikuwa ni tishio kubwa la afya kwa wananchi walio wengi.

"Wananchi walikuwa na uhitaji mkubwa wa maji safi na salama, hivyo tunaomba kama inawezekana, kuongezewa tanki lingine ili maji yawafikie wananchi wengi zaidi katika vijiji vya jirani, kwa kuwa kisima hicho kina maji mengi na ya kutosha ". Amesisitiza Mwenyekiti huyo wa kijiji.

Awali shirika la WAMATA licha ya kutekeleza mradi wa maji, lakini pia limeanza kuwahudumia vijana 10 watakaopewa mafunzo ya ushonanaji na kuchomelea vyuma lengo kuu ni kupambana na ukosefu wa ajira nchini.


ARUSHA DC

TUPO KAZINI✍✍


PICHA ZA MATUKIO WAKATI WA UZINDUZI WA MRADI WA MAJI KITONGOJI CHA NYAMAGANA






Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.