NA JULIUS LAIZER AFISA HABARI ARUSHA DC:
Wazazi na Walezi wenye watoto waliofaulu na kupangiwa kujiunga na elimu ya sekondari Halmashauri ya Wilaya ya Arusha wametakiwa kuhakikisha kuwa watoto wao wanaripoti shuleni kufikia tarehe 19/01/2024 ili kuendelea na masomo yao.
Haya yameelezwa na Afisa Elimu Sekondari Halmashauri ya Wilaya ya Arusha Ndugu Menard M. Lupenza alipokuwa akitoa taarifa ya Mapokezi ya wanafunzi waliofaulu na kuchaguliwa kujiunga na elimu ya Sekondari kidato cha kwanza kwa mwaka 2024.
Amesema kuwa jumla ya Wanafunzi wapatao 8966 walifaulu na kuchaguliwa kujiunga na masomo ya Kidato cha kwanza 2024 ikiwa idadi ya wavulana ni 4177 wasichana 4789 na kusema kuwa ufaulu huo umechangiwa na ushirikiano mzuri wa waalimu na wazazi katika maandali mbali mbali.
Ameeleza kuwa jumla ya Wanafunzi wapatao 5147 wameripoti shuleni kufikia hii leo tarehe 16/01/2024 idadi ya Wavulana ikiwa ni 2384 idadi ya Wasichana ni 2760 Wanafunzi watatu wenye mahitaji Maalum, sawa na asilimia 57.04.
Tangu tarehe 08/01/2024 shule zote za Halmashauri ya Wilaya ya Arusha imeendelea na zoezi la kuwapokea wanafunzi kwa usaili na kuanza masomo yao ya kujengewa Uwezo na kuzoeshwa Mazingira ya Elimu ya Sekondari kwa kufundishwa somo maalumu English Orientation Course, Hivyo Wazazi wahakikishe wanawapeleka Watoto wao shule.
Amesema Serikali ya Awamu ya Sita ya Mheshimiwa Rais Daktari Samia Suluhu Hassan imetoa fursa kwa Wazazi na Walezi kuhakikisha wanawapeleka watoto wao shule kwa kuwa Miundo mbinu ya kuwapokea wanafunzi imekamilika kwa asilimia mia moja, miundo mbinu hiyo ni Madarasa, Maabara, Samani, Waalimu na Mazingira mazuri ya Ufundishaji.
Amewajulisha Wazazi kuwa serikali Sikivu ya Mheshimiwa Daktari Samia Suluhu Hassan inaendelea kutekeleza mpango wake wa kutoa Elimu bila Malipo kwa Wanafunzi wa Darasa la Awali hadi kidato cha Sita lengo ikiwa ni kila mwanafunzi kupata elimu na kutimiza ndoto na malengo yake.
Amesema jukumu la azazi ni kuhakikisha wanawatimizia watoto wao Mahitaji yao Muhimu ya shule kama vile Sare, Madaftari,Usafiri wa kwenda Shule na kuhakikisha mwanafunzi anapata Chakula itakayomfanya aweze kuwa na Usikivu mzuri awapo Darasani.
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.