Na. Elinipa Lupembe.
Wananchi wa kata ya Kiutu halmashauri ya Arusha, wamejumuika kwa umoja wao, bila kujali rika wala jinsia zao, wakiwemo wazee, vijana na wanawake, kusafisha eneo lenye ukubwa wa takribani mita za mraba 1,777.5, eneo lililotolewa na wananchi wa kata hiyo, kwa ajili ya ujenzi wa shule ya sekondari ya kata, iliyopewa jina la Kiutu Secondary School.
Wananchi hao wamefikia uamuzi wa kujitokeza kulisafisha eneo hilo, ikiwa ni maandalizi ya ujenzi wa shule hiyo, mara baada ya Serikali kutoa fedha kiasi cha shilingi milioni 470, kwa ajili ya ujenzi wa shule ya Sekondari Kiutu, na wananchi wenzao kutoa eneo hilo, kata ambayo haijawahi kuwa na sekondari tangu kupatikana na kwa Uhuru wa Tanganyika.
Wananchi hao, wameweka wazi hisia zao za furaha, huku wakimshukuru Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, mama Samia Suluhu Hassan, kwa kusikia kilio chao cha muda mrefu kwa kuwapatia fedha hizo za ujenzi wa shule ya sekondari katika kata yao, kata ambayo haikuwahi kuwa na shule ya sekondari, licha ya kwamba mpango wa serikali ni kuwa na shule ya sekondari kwa kila kata.
"Tunamshukuru na kumpongeza sana mama Samia kwa kutuona sisi wananchi wa Kiutu, kwa miaka mingi sasa, tumekuwa tukichangia fedha za ujenzi wa madarasa kwenye shule zilizopo kwenye kata nyingine, mpaka ilifikia mahali ambapo tulikata tamaa ya kuendelea kutoa michango kwenye shule hizo, huku watoto wetu wakipata tabu kufuata elimu ya sekondari kwenye kata hizo, kwa sasa tunaamini watoto wetu hawatanyanyasika tena, watasoma hapa hapa nyumbani" wamesisitiza wananchi hao
Wananchi hao zaidi wamewashukuru wananchi wenzao wanne wenye imani na moyo wa kipekee na uzalendo, kwa kutoa eneo hilo, huku shukrani zaidi zikielekezwa kwa Mheshimkwa Diwani wa kata ya Kiutu, Mheshimiwa Malaki Malambo, ambaye ametoa eneo lenye ukubwa wa mita za mraba 6,401 na wengine kutoa mita za mraba 5,376.2, eneo ambalo kata hiyo haikuwa nalo.
Hata hivyo wananchi hao, wamesisitiza kuwa wako tayari, kuendelea kujitoa kuchangia nguvu kazi, wakati wote wa utekelezaji wa mradi huo wa ujenzi wa shule, huku wakisisitiza kuwa wako tayari kufanya kazi zote za mikono watakazoelekezwa na watalamu wahandisi wa majengo hiyo.
Naye Mkurugenzi Mtendaji, halmashauri ya Arusha, ameungana na wananchi hao katika zoezi la kusafisha eneo hilo, huku akiwapongeza kwa juhudi walizozionesha na kuwataka kuendelea kujitolea katika hauta zote za ujenzi wa shule hiyo mpaka hapo watoto wao, watakapoingia darasani.
Aidha mkurugenzi Msumi, amethibitisha halmashauri kupokea fedha kiasi cha shilingi milioni 470, kutoka Serikali Kuu, kupitia miradi yaake ya SEQUIP, kwa ajili ya kutekeleza mradi wa ujenzi wa shule ya sekondari Kiutu.
"Serikali imeelekza matumizi ya fedha hizo, shilingi milioni 470, kutumika kujenga jengo la ghorofa litakalobeba vyumba 8 vya madarasa, Maabara tatu za masomo ya Sayansi, maabara ya somo la Kompyuta (ICT), Matundu 20 ya vyoo vya wanafunzi pamoja na mfumo wa kuvunia maji ya mvua, wenye matanki mawili ya lita elfu 10 kwa kila moja" amefafanua Mkurugenzi Msumi.
Halmashauri ya Arusha inawashukuru na kuwapongeza wananchi hao, waliokubali kutoa eneo hilo kwa makubaliano ya kufidiwa eneo jingine katika eneo la Gomba Estate lililopo kata ya Mlangarini, kwa pamoja wakiwa na lengo la kuunga mkono juhudi za serikali katika sekta ya elimu, kwa kuwezesha uwepo wa shule ya kata katika kata ya Kiutu kama ilivyo kwa kata nyingine nchini.
ARUSHA DC
KaziInaendelea✍✍✍
PICHA ZA MATUKIO WANANCHI WAKISAFISHA ENEO.
Wananchi wa Kiutu waking'o visiki, kwa lengo la kusafisha eneo tayari kwa kutekelza mradi wa ujenzi wa shule yao ya Kata, shule ya Sekondari Kiutu.
Mkurugenzi Mtendaji, halmashauri ya Arusha, Seleman Msumi, ameungana na wananchi wa Kiutu, waloojitokeza kusafisha eneo tayari kwa kuanza utekelzaji wa mradi wa kujenga shule ya Sekondari Kiutu, Mkurugenzi huyo akichimba kisiki.
Wananchi wa Kiutu waking'o visiki, kwa lengo la kusafisha eneo tayari kwa kutekelza mradi wa ujenzi wa shule yao ya Kata, shule ya Sekondari Kiutu.
Wananchi wa Kiutu wakipambana kusafisha eneo, tayari kwa kutekelza mradi wa ujenzi wa shule yao ya Kata, shule ya Sekondari Kiutu.
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.