• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WATEKELEZAJI WA ZOEZI LA ANWANI ZA MAKAZI ARUSHA DC WATAKIWA KUTEKELEZA ZOEZI HILO KWA WELEDI

Posted on: March 12th, 2022

Watalamu watakaoshiriki kwenye zoezi la kitaifa la ukusanyaji na upangaji wa Anwani za Makazi, halmashauri ya Arusha, wametakiwa kufanya kazi hiyo kwa weledi na kuweka uzalendo mblele huku wakizingatia umuhimu wa zoezi hilo kwa maendeleo ya wananch na Taifa kwa ujumla.

Hayo yamesemwa Kaimu Mkurugenzi halmashauri ya Arusha, na Afisa Maendeleo ya Jamii, Angela Mvaa, wakati wa semina elekezi, iliyotolewa kwa watekelezaji wa zoezi la Anwani za Makazi wa kata ya Kiutu, semina iliyofanyika kwenye ofisi ya kata ya Kiutu.

Kaimu Mkurugenzi huyo, amewataka watalamu wote waliochaguliwa kutekeleza zoezi la upangaji wa Anwani za Makazi katika halmashauri ya Arusha, kuhakikisha wanatekeleza zoezi hilo kwa weledi kwa kuzingatia maelekezo, miongozo na taratibu walizopatiwa wakati wa mafunzo.

"Kila mshiriki wa zoezi hili anapaswa kutambua umuhimu wa zoezi hili kwa Taifa, na kutambua kuwa serikali imewaamini kuwapa kufanya kazi hiyo muhimj, hivyo mnapaswa kufanya kazi hiyo kwa weledi mkubwa na kuhakikisha taarifa za wamiliki wa makazi yote zimeingia kwenye mfumo pamoja na makazi yote kupatiwa namba" amefafanua Kaimu Mkurugenzi huyo.

Aidha mafunzo hayo, yaliambata na mafunzo kwa vitendo ya namna ya kujaza taarifa za mmiliki wa makazi kwenye fomu maalum pamoja na namna ya kuandika na kubadika namba kwenye nyumba, ambapo Kaimu Mkurugenzi huyo alianza kwa kuandika nyumba namna 1 kwenye kitongoji cha Engorika kata ya Kiutu.

Hata hivyo Kaimu Mkurugenzi huyo amewataka wananchi na wakazi wote wa halmashauri ya Arusha, kutoa ushirikiano watalamu na viongozi wa maeneo yao, watakaopita kwenye makazi yao kwa kuwapa taarifa sahihi zinazohitaji, lengo likiwa na kurahisisha zoezi pamoja na kukamilisha kwa wakati.

Naye Mratibu wa Anwani za Makazi, halmashauri ya Arusha, Loth Zachari ameweka wazi kuwa, mafunzo hayo, yenye lengo la kuwajengea uwezo watalamu wote wa ngazi ya kata, vijiji na vitongoji wataoshiriki katika utekelezaji wa zoezi hilo la Anwani za makazi, wakiwemo watalamu wa ngazi ya kata na vijiji, Maafisa watendaji wa kata na Vijiji,  Wenyeviti wa vijiji na vitongoji pamoja na vijana waliopatiwa ajira za muda. 

Mratibu huyo ameweka wazi kuwa, zoezi hilo linategemea kutekelezwa katika kata zote 27, vivijiji 67 na vitongoji 256 vya halmashauri ya Arusha na kuwataka wananchi wote kuhakikisha wanatoa ushirikiano kwa watalamu watakaopita kwenye Makazi yao kukusanya taarifa na kuandika namba kwenye nyumba zao.

ARUSHA DC

KaziInaendeleaa✍✍✍








Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.