• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WAZAZI NA WALEZI WATAKIWA KUTIMIZA MAJUKUMU YAO, KWA KUWAPA WATOTO WA KIKE MAHITAJI YAO MUHIMU

Posted on: July 13th, 2020

Na. Elinipa Lupembe.

    Wazazi na walezi wametakiwa kutimiza majukumu yao, ya kuwahudumia watoto wao hasa watoto wa kike, kwa kuwapungumzia muda wa kufanyakazi za nyumbani pamoja na kuwapatia watoto hao, mahitaji yote muhimu  ya shule ili kuwaepusha na viishawishi, wanavyokumbana navyo kutoka kwa wanaume, lengo ni kuwawezesha kujielekeza zaidi kwenye masomo.

    Rai hiyo imetolewa na Afisa Elimi Msingi, halmashauri ya Arusha, mwalimu Hosein Mghewa, alipokuwa akifungua na kufunga kikao kazi, kilichohususha wadau ya masuala ya  kupinga ukatiki dhidi ya watoto wa kike, kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa halmashauri hiyo.

     Mghewa amesema kuwa, watoto wa kike wanakutana na vikwazo vingi sana katika kipindi chao cha masomo, huku wazazi na walezi wakiwa chanzo cha vikwazo hivyo, kwa kutotimiza majuku yao kwa watoto hao, hasa kutowapatia mahitaji yao ya muhimu shuleni.

    Imeelezwa kuwa baadhi ya wazazi na walezi wameshindwa kutekeleza majukumu yao, badala yake, kuwaachia watoto wa kike kufanyakazi za nyumbani kabla na baada ya muda wa shule pamoja kushindwa kuwapa mahitaji yao muhimu ya shule, jambo linalosababisha wasichana kushawishiwa na zawadi mbalimbali kutoka kwa wanaume, na kujikuta wakijiingiza kwenye vitendo vya ngono, na kuweka kando masuala ya shule.

    Amewataka wazazi na walezi kutimiza majukumu yao ya malezi kwa watoto wa kike, licha ya kuzungumza na watoto wao na kuwajengea uwezo wa kujiami, lakini pia wanapaswa kuwapunguzia kazi za nyumbani na kuwapatia mahitaji muhimu, jambo amabalo litawaepusha wasichana, kuingia kwenye mitego na vishawishi vya zawadi katoka kwa wanaume.

     "Wazazi na walezi msikwepe majukumu yenu, wahudumieni watoto wenu hata kama hali ni ngumu, unakuta mtoto anafanyishwa kazi nyingi asubuhi, anakwenda shule kwa kuchelewa, hana mafuta ya kujipaka, vitaulo vya hedhi, hana kalamu wala daftari, inamlazimu kujitafutia yeye mwenyewe, jambo ambalo ni rahisi kwa mtoto huyu kushindwa kuepuka vishawishi, pindi akutanapo na mwanamme  wa kumpatia vifaa hivyo, " amesema Afisa Elimu huyo.

     Hata hivyo walimu, walioshiriki kikao kazi hicho, wamekiri baadhi ya wanafunzi kutokuwa na vifaa vyote vya shule, ikionesha dhahiriwazazi kutokwapatia watoto wao, mahitaji muhimu ya shule, huku watoto hao wajihangaikia kupata mahitaji hayo kwa kufanya vibarua au kuomba kwa wenzao.

    Aidha walimu hao wamethibitisha kuwepo tofauti kubwa ya kimasomo kati ya mtoto ka kike na wakiume, inayotokana na mila na desturi, huku wakilalamikia wazazi kuwapa kazi nyingi watoto wa kike kabla na baada ya kutoka shuleni, jambo linasababisha wasicha kukosa muda wa kujisomea wawapo nyumbani, tofauti na watoto wa kiume.

     Wameongeza kuwa mila na desturi za kabila la kimaasai, mtoto wa kiume akishatahiriwa, haruhusiwi kufanyakazi za nyumbani, hivyo majukumu yote yanamuangukia mtoto wa kike, huku mtoto wa kiume akiwa na muda mwingi wa kujisoma na mtoto wa kike akikosa muda wa kujisomea awapo nyumbani.

     Naye mwalimu John Mduma wa shule ya sekondari Ilkiding'a, amethibitsha kuwa, baadhi ya wanafunzi shuleni hapo, hawana vifaa vyote vya shule, na kuthibitisha baadhi ya wazazi kishindwa kitimiza mahitaji muhimu ya mtoto jambo ambalo linasababisha watoto kuingia kufanya vibarua ili wapate mahitaji huku baadhi ya watoto wa kike wakiinhia kwenye vitendo vya ngono.

    Ameweka wazi kuwa, endapo wazazi na walezi wataona umuhimu wa kuwapa watoto mahitaji yao muhimu ya shule, watoto watajikita zaidi kwenye masomo na kujiepusha na vitendo vya ukatili wa kingono.

   Hata hivyo wanafunzi waliohudhuria kikao kazi hicho, walipata fursa ya kueleza changamoto zinazowakabili watoto wa kike na kuwaomba walimu kupunguza ukali dhidi ya wasichana, badala yake kuchukua muda kuwasikiliza changamoto zinazowakabili, na kuwasaidia kuzitatua kwa njia sahii, wakiamini  kuwa ikiwa nyumbani wazazi wao, hawana uelewa  juu ya elimu ya mtoto wa kike, hivyo tegemeo kubwa la watoto hao ni walimu wao.

      Wamesema kuwa mila na desturi za kabila lao msichana huchumbiwa akiwa mdogo, mchumba akitaka kumchukua binti wazazi humlazimisha mtoto kuolewa na hata akipata ujauzito wazazi humfundisha mtoto kutokumtaja aliye mpa ujauzito, kitu kinachosababisha wasichana wengi kukatishwa masoma, kupoteza haki na kupoteza  ndoto zao.

     Awali kikao kazi kazi hicho kimeandaliwa na shirika la CWDC, lengo likiwa ni kutambulisha Mradi wa Kuwajengea Uwezo watoto wa kike kupinga ukatili wa kijinsia katika kata za 7 za Ilkiding'a, Kimnyaki, Bangata, Olkokola, Mwandet, Oloirien na Olturoto katika shule sekondari na msingi zilizopo katika kata hizo.

    Mradi huo utatekelezwa  kwa kipindi cha miezi sita kianzia sasa,  kwa ushirikiano wa Halmashauri ya Arusha na shirika la CWCD kwa ufadhili wa  Foundation for Civil Society Tanzania.




Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.