• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WAZIRI OR-TAMISEMI:WAOMBAJI 18,449 WAPATA AJITA NA KUPANGIWA VITUO VYA KAZI

Posted on: June 5th, 2023

Waziri wa Nchi, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Angellah Kairuki ametangaza waombaji 18,449 wa ajira mpya waliochanguliwa na kupangiwa vituo vya kazi katika kada ya ualimu na afya huku akitoa maelekezo nane mahsusi.


Mhe. Kairuki akizungumza Juni 5, 2023 jijini Dodoma kuhusu ajira mpya 21,200 zilizotangazwa Aprili 2023, amesema kati ya waombaji hao 18,449 waliochaguliwa 5,319 ni wa kada za afya na kada za ualimu ni 13,130.


“Mtakumbuka Mtakumbuka kuwa mwezi Aprili, 2023; Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, alitoa kibali cha ajira ya watumishi 21,200 kati yao 13,130 walikuwa wa kada ya Ualimu na 8,070 wa kada za Afya.”


“Hata hivyo, mchakato wa kukamilisha uchambuzi wa maombi katika jumla ya nafasi 2,751 za kada ya afya unaendelea, na utatangazwa punde utakapokamilishwa,”amesema.


Waziri Kairuki amesema katika maombi 171,916 yaliyopokelewa waombaji 86,448 waliokidhi vigezo na 18,449 ndio walichaguliwa na kupangiwa vituo vya kazi.


Amewaagiza waajiriwa wapya kabla ya kuripoti kwenye vituo vya kazi walivyopangiwa, wanatakiwa kuripoti kwa Wakurugenzi wa Halmashauri na nyaraka halisi na atakayechukua posho ya kujikimu na baadaye asiripoti katika kituo chake cha kazi alichopangiwa atachukuliwa hatua stahiki kwa mujibu wa sheria ikiwa ni pamoja na kushtakiwa kwa kosa la kujipatia fedha au mali kwa njia ya udanganyifu.


“Waajiriwa wapya ambao hawataripoti katika vituo walivyopangiwa ndani ya siku 14 kuanzia tarehe ya tangazo hili, watakuwa wamepoteza nafasi zao na nafasi hizo zitajazwa na waombaji wengine wenye sifa waliopo kwenye kanzidata ya Ofisi ya Rais – TAMISEMI,”amesema.


Pia amesema waajiriwa hao hawaruhusiwi kubadilisha kituo na kuomba uhamisho kabla ya kutimiza miaka mitatu, watatakiwa kusaini mkataba wa kufanya kazi katika vituo hivyo si chini ya miaka mitatu.


Mhe.Kairuki amewaelekeza Wakurugenzi wa Halmashauri ambazo waajiriwa wapya wamepangiwa kuhakikisha wanawawezesha wa kuzingatia sheria, kanuni, taratibu na miongozo ya utumishi wa umma na baadaye kutoa taarifa ya kuripoti kwa watumishi hao.


Naye, Mkurugenzi wa Idara ya Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe kutoka TAMISEMI, Dk. Ntuli Kapologwe amefafanua ajira za kada za afya ambazo zitatangazwa tena kutokana na kukosa waombaji wenye sifa stahiki kuwa ni za Wataalamu wasaidizi wa viungo, wataalamu wa kuendesha mitambo ya x-ray na Maofisa Tabibu wasaidizi kwa ngazi ya astashahada ambao uzalishaji wake bado ni mdogo.


SOURCE :ORT- TAMISEMI


Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.