Na.Elinipa Lupembe
# Amewashukuru wananchi wa mkoa wa Arusha kwa amani na utulivu uliopo, ameshukuru kwa mapokezi mazuri aliyoyapata Arusha na amewataka wananchi wa Arusha kuendelea kuchapa kazi kwa bidii ili kujenga nchi.
# Ninafahamu Arusha kuna tatizo kubwa la miundombinu ya barabara, serikali imejipanga, kuunganisha barabara za wilaya na tumeongeza uwezo mkubwa kwa TARURA, uwezo wa fedha na utalamu pia, kwa lengo la kuboresha barabara za ndani zinazolalamikiwa, barabara za vumbi zitengenezwa kwa kiwango cha changarawe, tunataka barabara hizo zipitike kwa miongo yote, iwe mvua iwe jua na mazao ya wakulima yafike barabarani.
# Tumejipanga kudhibiti uuzaji holela wa madini yetu ya Tanzanite, ili kurudisha hadhi yake ambayo ilipotea pamoja na kuyapandisha thamani, kutoka na ukweli kwamba Tanzanite inapatikana na Tanzania peke yake na si nchi nyingine kama ilivyokuwa inafahamaika hapo awali, kwa kufanya hivi, tunategemea bei ya Tanzanite itapanda katika soko la dunia.
# Tunafahamu maradhi ya UVIKO 19 yameathiri sana sekta ya Utalii, ambayo ni sekta tegemezi hapa Arusha, lakini serikali imefanya jitihada kubwa katika kurejesha hali ya utalii nchini, kwa kuingiza chanjo ya UVIKO 19 na wananchi kuanza kuchanja, Chanjo tulizopokea kwa awamu ya kwanza tumekamilisha kwa asilimia 80, hii imefanya nchi yetu kuondolewa kwenye orodha ya nchi ambazo hazitembeleki, juzi tumepokea ndege mbili kubwa zenye watalii 200 wamekuja Arusha na wengine wamekenda Zanzibar.
# Tumepata Wawekezaji wa kujenge mahoteli ya kitalii ya nyota 5, ili watalii wakifika nchini wapate pahala pa zuri pa kufikia.# Tumetenga fedha za kiasi cha shilingi bilioni 90.2, zitumike katika shughuli mbalimbali za kuboreshaa sekta ya Utalii, tumetengeneza Filam maalum ya kuutangaza utalii kwa konesha vivutio vinavyopatikana Tanzania, tuendelee kuwa wavumilivu, hali ya utalii itarudi kuwa nzuri kwani watalii wameanza kuingia nchini.
# Serikali iko kwenye mpango wa kufufua viwanda vilivyokufa ndani ya mkoa wa Arusha, kwa kuweka makonga ya viwanda, kiwanda cha Matairi 'GENERAL TYRE' kutakuwa na viwanda 20 ndani yake, ikiwemo kiwanda cha kuzalisha mipira, hii itakuza ajira kwa watu wetu na kukuza uchumi.
# Tunafahamu changamoto wanayoipata wananchi wa wilaya ya Arumeru, changamto hiyo ipo katika wilaya nyingi zenye maeneo makubwa kiutawalai lakini kwa sasa Seriali haitashughulika na ugawanyaji wa maeneo ya kiutawala kutokana na gharama kubwa za kugawanya maeneo hayo, niwaombe tujikite kwanza kwenye kupandisha uchumi wetu ambao umeshuka kutokana na athari za UVIKO 19.
# Ninafahamu changamoto za vijana, mama yenu silali kutokana na changamoto zinazowakabili vijana wangu, tumepata Mwekezaji wa kujenga chuo cha TEHAMA ambapo vijana watajifunza ujuzi wa masuala ya teknolojia, bado tunatafuta njia muafaka ya kutatua changamoto za vijana nchini.
# Ziara zangu kwa nchi za jirani zina lengo la kuondoa vikwazo, vilivyokuwepo na nchi hizo, biashara kati ya Kenya na Tanzania imefunguka na imekua zaidi ya mara sita.
#KaziIendelee ✍✍✍
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akihutubia wananchi wa mkoa wa Arusha kwenye uwanja wa Sheik Amri Abeid wakati wa ziara yake ya kikazi mkoani Arusha.
Mkuu wa mkoa Arusha, Mhe. John Mongela akizungumza na wananchi wa mkoa wa Arusha kabla ya kumkaribisha Mhe, Rais kuhutubia hadhara ya wakazi wa Arusha waliofika kwenye uwanja wa Sheik Amri Abeid.
Katibu wa Chama Cha Mapinduzi Taifa, Komredi Daniel Chongolo akizungumza na wakazi wa mkoa wa Arusha waliofika kwenye uwanja wa Sheik Amri Abeid, wakati wa ziara ya mheshimiwa Rais mkoani Arusha,
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.