• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Waendesha Bodaboda Arusha, kuanza rasmi kupambana na Ukatili dhidi ya Watoto

Posted on: September 9th, 2019

Na. Elinipa Lupembe.

Viongozi wa umoja wa waendesha bodaboda Arusha (UWABA), wamekubaliana kuanza rasmi, kuwajibika katika kulinda haki na usalama wa watoto, wakiwa katika kazi zao, kufuatia mafunzo waliyoyapata ya Ulinzi na Usalama wa Mtoto yenye ujumbe usemao, 'Bodaboda Usafiri Salama, Tulinde Haki za Watoto'.

Waendesha Bodaboda hao, wamekubaliana hayo, baada ya kupata mafunzo ya siku moja, yaliyohusu wajibu wao,  katika ulinzi na usalama wa mtoto,  mafunzo yaliyofanyika kwenye ukumbi wa mikutano, halmashauri ya Arusha, kwa udhamini wa shirika la CWDC la Jijini Arusha.

Madereva hao wamekiri kuwa awali, hawakufahamu sana, juu ya ulinzi na usalama wa mtoto na kuwa wao wanahusika sana kuwalinda, kutokana na ukweli kuwa, wamekuwa wakiwapakia watoto kwenye kazi zao, bila kuelewa kuwa wanajukumu la kuwalinda na kuwahakikishia usalama wao wakati wote.

Wamesema kuwa, wanaishukuru Serikali kwa kutambua umuhimu wa kundi hilo, na kuanza kulishirikisha kwenye mambo ya kijamii, kwa kuwapa mafunzo mbalimbali yanayowezesha kundi hilo kujitambua, kujithamini na kuanza kuthaminika na jamii kwa sasa.

Mwenyekuti wa UWABA Arusha, Goodluck Ndibalema, amesema kuwa, ameanza kuona mabadiliko makubwa ya kitabia kwa vijana waendesha bodaboda, kutokana na ushirikishwaji unaofanya na Serikali ya awmu ya tano kwa kushirikiana na mashirika yasiyo ya kiserikali, hali iliyowafanya vijana wa kundi hilo, kujitambua na kujiona kuheshimika na kuthaminika na jamii inayowazunguka licha ya changamto mbalimbali zinazowakabili.

"Kundi la waendesha Bodaboda, limekuwa likidharaulika kutokana na kundi hilo kutengwa na kutokushirikishwa kwenye mambo ya kijamii, na kuonekana kama ni kundi la wahalifu, ninakiri kwa sasa kutokana na ushirikishwaji unaofanywa Serikali ya awamu ya tano, waendesha Bodaboda wamebadilika na kujitambua kuwa, wanajukumu kubwa kwa jamii" amesema Rugemalila

Naye mkurugenzi mtendaji, halmashauri ya Arusha,Dkt. Wilson Mahera, amewahakikishia madereva Bodaboda hao kuwa, Serikali ya awamu ya tano, inatambua huduma wanayoitoa kwa jamii, na kuwataka kupambana na vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto, kwa kuwalinda na  kutoa taarifa pindi wanaposikia au kuona watoto wakifanyiwa ukatili.

Amesema kuwa, kuanzia sasa Bodaboda uwe usafiri salama na kuzuia ulatili kwa watoto, kwa kuwa, baadhi yao wamekuwa wakishutumiwa kutumia usafiri wao kuwashawishi watoto wa shule na kuwasababishia mimba na ndoa za utotoni.

Naye Mwenyekiti wa halmashauri ya Arusha, mhe. Noah Lembris, amewasisitiza madereva hao, kufuata sheria za usalama barabarani, wanapoendesha pikipiki zao, ili kuzuia ajali, zinazosababisha vifo na pengine ulemavu, kwa kufanya hivyo ni kuzuia ukatili kwa watoto kwa kuwa vifo hivyo husababisha watoto wengi kubaki yatima.


Akieleza lengo la kukutana na waendesha Bodaboda hao, mkurugenzi wa Shirika la CWCD, Hindu Mbwego, amesema kuwa, lengo kuu ni ushirikishwaji na kuwapa mafunzo ya Ulinzi na usalama wa mtoto, yatakayowawezesha kushiriki katika kuzuia ukatili kwa watoto, kwa kuwa, baadhi ya waendesha Bodaboda wamekuwa, wakilaumiwa kwa kutumia vyombo hivyo kuwarubuni wanafunzi na kutumia usafiri huo kuwapeleka kwenye matukio ya ngono.

Amewataka madereva hao, kuona thamani ya watoto hao, na kuacha tabia ya kutumika kuwapeleka watoto kwenye nyumba za wagenj, na badala yake kushiriki kuwalinda watoto, pamoja na kutoa taarifa za matukio hayo, ili kuifanya jamii kuona Bodaboda ni Usafiri salama unaozuia ukatili dhidi ya watoto.

Awali, Mafunzo hayo, yamekuwakutanisha Viongozi wa Vituo vya Bodaboda, kutoka halmashuri mbili za Jiji la Arusha na Halmashauri ya Arusha na yaliambatana na maandamano ya kuzunguka jiji la Arusha, yakiwa na Kauli mbiu ya BODABODA USAFIRI SALAMA, ZUIA UKATILI DHIDI YA WATOTO.







Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.