• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Historia


HISTORIA YA HALMASHAURI YA WILAYA YA ARUSHA.

Karibu Halmashauri ya Arusha kufahamu Historia fupi ya Halmashauri hii ikiwemo Halmashauri Chimbuko, ukubwa wa eneo na maeneo ya kiutawala ikiwemo Tarafa, Kata, Vijiji na Vitongoji, mipaka yake, Jiografia ya mahali ilipo, Uongozi kiutawala, Idadi ya watu, wenyeji wa halmashauri ya Arusha, shughuli wanazofanya wenyeji. Mahali zilipo Ofisi za Makao Makuu ya halmashauri ya Arusha. Pamoja na Dira, Maono, Malengo na Mikakati ya Halmashauri kwa kipindi cha Miaka Mitano.

MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI YA WILAYA YA ARUSHA:

Ofisi Za Makao Makuu ya Wilaya ya Arusha zipo Kata ya Kiutu Kijiji cha Engorika eneo la Sekei Mkabala na Hoteli ya Kimataifa ya Mount Meru umbali wa takribani mita 300 kutoka barabara kuu ya Moshi – Arusha- Namanga.

CHIMBUKO LA HALMASHAURI YA ARUSHA:

Halmshauri ya Wilaya ya Arusha ilianza rasmi tarehe 01.07.2007 baada ya kugawanywa iliyokuwa Halmashuri ya Meru na kuwa na Halmashauri mbili za Halmashauri ya Meru na Halmashauri ya Arusha.

Halmashauri ya Arusha ni miongoni mwa Halmashauri saba za mkoa wa Arusha inapatikana chini ya Mlima Meru ikiwa imepakana na halmashauri ya Meru kwa upande wa Mashariki, Halmashauri ya Monduli upande wa Magharibi, Halmashauri ya Longido upande wa Kaskazini Magharibi, Halmashauri ya Simanjiro mkoa wa Manyara kwa upande wa Kusini. Halmashauri ya Arusha imelizunguka jiji la Arusha kwa pande zake zote.

Halmshauri ya Arusha ina eneo lenye ukubwa wa Kilomita za mraba 1446.692 inapatikana Magharibi mwa mlima Meru wenye urefu wa mita 4,562 kutoka usawa wa bahari ambao ni mlima wa pili kwa urefu Tanzania baada ya mlima Kilimanjaro wenye urefu wa mita 5,890.

Halmashauri ya Arusha imelala kati ya Latitudo 3000- 3040’ Kusini mwa Ikweta na Longitudo 36015’-360 55’   Mashariki.

UKUBWA WA ENEO: 

Wilaya ina eneo la kilomita za mraba 1,446.692. Matumizi makubwa ya ardhi katika Wilaya ni pamoja na: kilimo, makazi, biashara, madini, ufugaji / malisho, utalii wa asili na viwanda vidogo na biashara na hifadhi za misitu.

 Ambapo, hifadhi ya misitu ina eneo la kilomita za mraba 54.17, ardhi inayofaa kwa kilimo ni Kilomita za mraba 446.56, malisho huchukua eneo la Kilomita za mraba 506.01 sehemu ya ardhi iliyobaki yenye ukubwa wa wastani wa Kilomita za mraba 440.2 inatumika kwa shughuli nyingine kama vile biashara, makazi na madini.

ENEO LA UTAWALA:

Halmashauri ya Arusha ina tarafa tatu za Enaboishu, Moshono na  Mukulat ikiwa na kata 27 za Bangata, Bwawani, Ikiding’a, Ilboru,  Kimnyaki, Kiranyi, Kisongo, Kiutu, Laroi, Lemanyata,  Matevesi, Mlangarini, Mwandet, Moivo, Musa, Nduruma Oldonyosambu, Oldonyowas,  Olkokola,  Oljoro, Olmotony, Oloirieni, Olturoto, Olturumet, Sambasha, Sokon II na Tarakwa; Ikiwa na  Vijiji 67, Vitongoji 256 pamoja na  Mamlaka moja ya Mji Mdogo inayojulikana Mamlaka ya Mji Mdogo Ngaramtoni yenye kata 7 na Vitongoji 21.

Halmashauri ya Arusha ina Jimbo Moja la Uchaguzi la Arumeru Magharibi lenye Mbunge mmoja na Madiwani 36 kati ya hao Madiwani 27 ni wa kuchaguliwa na Madiwa 9 wakuteuliwa - Viti Maalum. Halmashauri ya Arusha inaongozwa na Mwenyekiti wa Halmashauri ambaye amechaguliwa na Madiwani 36.

HALI YA HEWA:

Halmashauri ya Arusha hii hupata mvua kwa wastani wa mm 500 hadi mm 1200 kwa mwaka. Hali ya hewa ya Halmashauri ya Wilaya ya Arusha ina sifa ya misimu miwili ya mvua, mvua za muda mrefu na mvua za vuli. Mvua za muda mrefu huanza mwezi Aprili hadi mwanzoni mwa mwezi Juni wakati mvua za vuli huanza mwezi Oktoba hadi Desemba ambazo ni kati ya mm 800 hadi mm 1000 kwa mwaka. Mvua za wastani kwa mwaka ni mm 900 zikiwa na kiwango cha chini cha unyevu wa asilimia 42 na kiwango cha juu cha unuyevu ni asilimia 50, wakati joto ni kati ya nyuzi 160C hadi nyuzi 330C mwaka mzima. Kasi ya upepo ni kati ya kilomita 6 na 7 kwa saa, hali ya hewa ya baridi hutokea katika miezi ya Juni hadi Agosti joto likiwa ni kati ya nyuzi 160C na 280C.

IDADI YA WATU:

Kutokana  na Sensa ya watu na Makazi ya mwaka 2012 halmashuri ya Arusha ina jumla ya watu 323,198 ikiwa wanaume 154,301 na wanawake 168,897 kwa ukubwa wa

277.4 ikiwa na ongezeko la asilimia 3.4%., Kaya 72,289 ikiwa na wastani wa watu watano kwa kaya.

WENYEJI WA HALMASHAURI YA ARUSHA:

Wenyeji asili wa Halmashauri ya Arusha ni Wamasaai na Wameru na wakazi wengine ni wachaga, wapare, wambulu, warangi, wanyeramba, Wagogo na wasuksuma waliohamia kutoka wilaya za mikoa ya jirani na mkoa wa Arusha kutokana na shughuli za biashara na za kijamii.

 

 

SHUGHULI ZA KIUCHUMI:

Sehemu kubwa ya wakazi wa Halmashauri ya wilaya ya Arusha wanajishughulisha na kilimo na ufugaji, Utalii, Biashara za Makampuni makubwa na madogo, Biashara ndogondogo na wajasiriamali wakubwa na wadogo. Aidha  wakazi wengine wana ajira katika: -

Katika uendeshaji wa biashara kuna zaidi ya biashara 1,500 zikiwemo maduka ya rejareja, migahawa, kuendesha nyumba za kulala wageni, machinjio, ususi, uuzaji wa mbao na nguzo, uuzaji wa vifaa vya ujenzi, mashine za kusaga, useremala, ujenzi, kutengeneza vifaa vya chuma n.k. Makampuni makubwa na madogo yanayojishughulisha na utalii (cultural tourism), ikiwa ni pamoja na uwindaji. Wakulima wadogowadogo wanaojishughulisha zaidi na kilimo cha mboga mboga na kukuza miche ya miti.

UONGOZI:

HISTORIA YA MWENYEKITI HALMASHAURI YA ARUSHA TANGU KUANZISHWA KWAKE MWAKA 2007:

Na.
Jina Kamili
Mwaka alioanza
Mwaka alioondoka
1.
Mhe. John Ole Saitabau
2007
2010
2.
Mhe. Simon Ole Saning’o
2010
2015
3.
Mhe. Noah L. Saputu
2015
-

 

HISTORIA YA WAKURUGENZI WA HALMASHAURI YA ARUSHA TANGU KUANZISHWA KWAKE MWAKA 2007:

Na.
Jina Kamili
Mwaka alioanza
Mwaka alioondoka
1.
Halfan H. Hida      
2007
2010
2.
Fidelis S. Lumato            
2013
2016
3.
Dkt. Wilson M. Charles  
2016
-


Julai Mosi 2017, Halmashauri ya Wilaya ya Arusha iliadhimisha  miaka 10 tangu kuanzishwa kwake kutokana na kugawanywa kwa Halmashauri ya Wilaya ya zamani ya Arumeru.

Mwaka 2017 halmashauri ya Arusha imeandaa Mpango Mkakati wa mika miatano kwa mwaka 2016/2017 - 2020/2021, kwa mujibu wa matakwa ya

Sheria Namba 9 ya mwaka 1982 ambayo inahitaji Serikali za Mitaa (Halmashauri) kuandaa Mipango Mikakati ya miaka mitano ili iweze kutumika kama miongozo wakati wa maandalizi yaa Mpango wa Muda wa Kati na Muundo wa Bajeti ya Matumizi (MTEF).

Mpango Mkakati ulianisha vipaumbele katika utoaji wa huduma na utaratibu wa kawaida wa mapitio ya kila mwaka uliofanywa na jamii.

Mpango Mkakati huu wa miaka mitano (2016/2017 - 2020/2021) una lengo la kukamilisha Dira ya Halmashauri ya Wilaya ya kuwa kuongoza Halmashauri iliyobadilishwa inayotoa huduma zenye ubora wa juu kwa ajili ya maendeleo endelevu ya jamii ifikapo mwaka 2025.

Mpango mkakati huu wa 2016 / 2017 - 202/2021 unasisitiza katika kuboresha utoaji huduma kwa jamii ya Wilaya ya Arusha kupitia matumizi sahihi na yenye ufanisi ya rasilimali.

MAONO:

Kubadili Jamii kwa kutoa huduma bora na kuleta maendeleo endelevu kwa Jamii ifikapo 2025.       

DIRA:

Kutoa huduma bora kwa kutumia rasilimali zilizopo kwa ufanisi ili kuleta tija na maendeleo endelevu kwa Jamii.


MALENGO MAHUSUSI:

  • Kuboreshahuduma na kupungua kwa maambukizi ya UKIMWI/VVU,
  • Utekelezaji na uendelezaji wa vita dhidi ya rushwa kwa ufanisi,
  • Kuboreka kwa upatikanaji wa huduma kwa bora na usawa,
  • Kuongezeka na kuboresheka kwa huduma za kiuchumu na miundombinu,
  • Kuboresheka kwa shughuli za utawala bora,
  • Kuimarika kwa ustawi wa Jamii, Jinsia na uwezeshaji wa Jamii,
  • Kuboresheka kwa utayari wa kukabiliana na majanga,
  • Kuimarika kwa usimamamizi na utunzaji wa mazingira na maliasili,
  • Kuimarika kwa teknolojia ya habari na mawasiliano.


  • MAADILI MAKUU
  • Kufanya kazi kwa umoja – Kufanya kazi kwa ushirikiano.
  • Uwazi na uwajibikaji – kutangaza maono na dira yetu vijulikane, kuwa na uelewa wa pamoja, kujenga uaminifu, kuwajibika kwa kila kwa nafasi zetu nk.
  • Matumizi ya rasilimali yenye tija na ufanisi–Kutumia rasilimali zilizopo kwa busara, kushirikiani kutumia rasilimali haba.
  • Kutokuwa na rushwa -  Kufanya Halmashauri kuwa sehemu isiyo na harufu ya rushwa ya aina yoyote.
  • Huduma bora kwa wateja/wananchi–kutumia lugha za staha na ukarimu, kutoa huduma zenye kuridhisha.
  • Ulinzi – kuwa na moya wa uzalendo, na ulinzi wa mali za Halmashauri.
  • Maamuzi yenye ushahidi – kuwepo kwa taarifa sahihi na za wakati, ushahidi.
  • Uaminifu na Usiri – Kuaminiana na kutunza siri za Halmashauri.
  • Uadilifu na ubora–kuwa waadilifu, kujali na kutoamsaada kwa wateja unahitajika n.k.

 

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI WA NAFASI ZA UDEREVA TAREHE 28/12/2018 December 19, 2018
  • MAADHIMISHO YA WIKI YA UNYONYESHAJI DUNIANI TAREHE 1-7, AGOSTI 2020. July 31, 2020
  • TANGAZO KWA WANANCHI WOTE MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI WA ROBO YA PILI 2O20/2021 TAREHE 29.01.2021 January 29, 2021
  • KINGA TIBA YA KICHOCHO NA MINYOO YA TUMBO KWA WATOTO MIAKA 5-14 March 02, 2021
  • Tazama zote

Habari mpya

  • DC ARUMERU ATEMBELEA MAENEO YALIYOPATA MADHARA YA MVUA ARUSHA DC..

    March 24, 2023
  • MVUA KUBWA YALETA MADHARA ARAFA YA MUKULAY ARUSHA DCA DC

    March 24, 2023
  • MVUA KUBWA YALETA MADHARA ARAFA YA MUKULAT ARUSHA DC

    March 24, 2023
  • DC ARUMERU AFANIKISHA MCHANGO WA MAZIWA YA MTOTO KWA KAYA ILIYOBOMOKEWA NYUMBA OLMOTONY

    March 24, 2023
  • Tazama zote

Video

MFUGAJI AKIELEZEA FAIDA ZA UHIMILISHAJI WA NG'OMBE WA MAZIWA - BANDA LA MIFUGO ARUSHA DC
Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.