• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Malaigwanani wakubali kupambana kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto

Posted on: July 31st, 2018

Na. Elinipa Lupembe.

Wazee wa koo na mila wa kabila la kimasai, maarufu kama Malaigwanani, halmashauri ya Arusha, wamekubaliana kupambana na kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto unaofanyika ndani ya jamii yao.

Wazee hao wamekubaliana hayo, wakati wa mafunzo ya siku moja yaliyojumuisha Wazee wa mila na viongozi wa dini, semina iliyofanyika kwenye Ukumbi mdogo wa Mwenyekiti, halmashauri ya Arusha.

Wazee hao wamekiri kuwepo kwa vitendo  hivyo vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto na kuthibitisha kuwa vitendo vingine hufanywa na jamii, kutokana na mila na desturi za kabila la kimasaai.

Wamefafanua kuwa, baadhi ya mila na desturi za Kimasai zimepitwa na wakati,  hivyo kama jamii, inapaswa kuachana nazo, kwa kuwa hazina faida, bali zina madhara makubwa kwa jamii yao.

Wazee hao wa mila wameongeza kuwa, licha ya kuwa bado mila hizo zinaendelea kufanyika wamethibitisha kuwa, kwa sasa vitendo hivyo vimeanza kupungua kwa kasi kubwa, kutokana na jamii hiyo sasa kupata elimu na kufahamu madhara ya mila hizo pamoja na sheria zinazozuia ukatili huo.

Hata hivyo wazee hao wamekiri kupambana kwa kasi na ukatili huo kwa kuifanya agenda ya kudumu kwenye vikao vyao vya mila, nyumbani na pindi wanapokutana na wananchi.  

Katibu Mkuu wa Ukoo wa Mollel Tanzania,  Laigwanani Saitabau Namoyo, amesema kuwa upambanaji wa mila potofu zinazowakandamiza mwanamke na mtoto hasa ukeketaji na ndoa za utotoni, imekuwa ni agenda ya kudumu inayozungumzwa kwenye vikao vya ukoo, huku wakiendelea kuelimishana taratibu kuanzia ngazi za familia.  

Mkuu huyo wa ukoo ameongeza kuwa, kwa sasa vitendo hivyo vimeanza kupungua sana, kutokana na ukweli kwamba, hata watoto wenyewe wanazitambua haki zao kwa kufundishwa shuleni.    

"Tangu serikali ilipoanzisha shule za kata, jamii ya kimasaai imeanza kupeleka watoto wa kike shule, mtoto mwenyewe akirudi nyumbani,tayari anajitambua na kuanza kutuelimisha madhara ya mila zinazowakandamiza hasa kukeketwa na ndoa za utotoni" amesema Laigwanani huyo.

Aidha ameitaka jamii kutokuichukulia jamii ya kimasaai kuwa ni katili, mila hizo wamezikuta na kuzirithi kutoka kwa babu zao, ingawa kwa sasa wametambua madhara ya mila hizo, huku wakiendelea kuelimishana taratibu  na kuachana nazo.

Naye Shehe wa msikiti wa Sambasha, Swalehe Jumanne,  amesema kuwa wamekuwa wakitoa elimu ya mapambano dhidi ya ukatili wa wanawake na watoto kwenye nyumba za ibada na kuwaelimisha watoto juu ya haki zao wakati wa vipindi vya madrasa.

Mkurugenzi washirika la Centre for Women and Youth Development (CWCD) Tanzania, mama Hindu Mbwego, amesema kuwa, lengo la mafunzo hayo ni kuwashirikisha viongozi hao wa jamii katika kutekeleza mapambano dhidi ya ukatili wa wanawake na watoto kwenye jamii zao.                                      

Ameongeza kuwa viongozi hao wa jamii,  wamejengewa uwezo wa namna sahihi ya kupambana na kuachana na mila hizo, na kuwa na uelewa wa pamoja namna ya kuwalinda watoto pamoja na kutoa taarifa pindi matukio ya ukatili yanapotokea.    

Afisa Maendeleo ya Jamii Halmashauri ya Arusha, Lovil Nguyaine amesema kuwa, mafunzo hayo yametolewa na halmashauri kwa kushirikiana na ASAS ya CWDC na jumla ya wazee thelathini wamejengewa uwezo wa mapambano  dhidi ya ukatili wa wanawake na watoto katika maeneo yao.

Amefafanua kuwa katika kata hizo kumi kila kata  imewakilishwa na Laigwanani mmoja na viongozi wa dini wawili kutoka kata za Mwandeti, Olkokola, Sambasha, Laroi, Lemanyata, Ilkiding'a, Kisongo, Musa, Matevesi na Oljoro.

Matangazo

  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI WA ROBO YA TATU 2O21/2022 tarehe 09.05.2022 May 08, 2022
  • Tazama zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI WA ARUSHA DC,BW.SELEMAN MSUMI AKIWA NA WATUMISHI WA HALMASHAURI HIYO KATIKA MASDHIMISHO YA MEI MOSI KIMKOA ARUSHA

    May 02, 2025
  • HERI YA MEI MOSI

    May 01, 2025
  • HERI YA SIKU YA MEI MOSI

    May 01, 2025
  • MHE. MAJALIWA MGENI RASMI KATIKA MAADHIMISHO YA SIKU YA UHURU WA VYOMBO VYA HABARI DUNIANI

    April 29, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.