• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

MKURUGENZI WA OPEC FUND ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA TASAF NCHINI

Posted on: March 29th, 2022

Na. Elinipa Lupembe.

Mkurugenzi wa Umoja wa Nchi zinazozalisha Mafuta kwa wingi Duniani (Opec Fund), Dkt. Alkhalifa Abdulhamid Saleh, amesema ameridhishwa na utekelezaji wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa na serikali, kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii - TASAF, kadhalika amesema Umoja huo utaendelea kushirikiana na serikali ya Tanzania kuhakikisha, miradi yote iliyofadhiliwa na OPEC FUND, inakamilika kwa wakati na kuleta matokeo chanya kwa jamii

Hayo aliyasema leo, wakati  akikagua miradi ya maendeleo ya inayotekelezwa na TASAF awamu ya III na ya IV, katika shule ya sekondari Oldonyowas, halmashauri ya Arusha, wilaya ni Arumeru, mkoa wa Arusha.

"Tunaishukuru serikali ya Tanzania kwa kushirikiana nasi, kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo ya kuondoa umasikini katika sekta ya elimu na afya, nimefurahi kuona watoto wanasoma katika mazingira bora kwenye madarasa mazuri na mabweni mazuri, shule ina jengo zuri la utawala pamoja na nyumba nzuri za walimu" amesistiza  Dkt. Alkhalifa 

Aidha, Dkt. Alkhalifa ameongeza kuwa, malengo ya serikali kuanzia mwaka 2020 -2025, ni kuhakikisha inapeleka maendeleo kwa kasi kwa wananchi lengo likiwa ni kukabiliana na wimbi la umasiki, kwa kuwezesha huduma za afya na elimu pamoja na kuwawezesha wananchi kukuza pato la familia kwa maendeleo ya jamii nzima.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF TANZANIA,  Ladislaus Mwamanga, amesema kuwa, ugeni kutoka OPEC FUND, umekuja kwa ajili ya kufanya mapitio ya kawaida pamoja na kufanya tathimini ya miradi iliyotekekelezwa na fedha kutoa OPEC FUND.

"Umoja huo unashirikiana serikali ya Tanzania kuchangia miradi ya maendeleo kwa wananchi kwa ajili ya kupunguza wimbi la umasikini katika jamii, hivyo wamekuja kuona miradi hiyo, kwa ujumla wake na wameona utekelezaji wa miradi na kuridhishwa na ujenzi wa miundombinu ambayo inawasaidia sana wanafunzi, kwa kuwa wanapata huduma zote za msingi shuleni" amesema Mkurugenzi Mwamanga.

Mkurugenzi Mwamanga, amefafanua kuwa, viongozi wa OPEC walipokutana na Mheshimwa Rais Samia Suluhu Hassan, walitoa mkopo wa dola za Kimarekani milioni 50 sawa na shilingi bilioni 120, kwa ajili ya kuendleza mradi wa kupunguza umasikini awamu ya nne, mradi ambao unatekelezwa katika mikoa mitano ya Tanzania Bara, ambayo ni Arusha Njombe, Simiyu, Mwanza na Geita.

Mwenyekiti wa Kijiji cha Oldonyowas, Mhe. Godfray Ayo, ameushukuru Umoja wa nchi hizo zinazozalisha mafuta kwa wingi, kupitia TASAF, kwa kutoa fedha, ambazo zimewezesha ujenzi wa miundombinu ya shule ya sekondari Oldonyowas, pamoja na fedha za kupunguza umaskini kwa wananchi wa eneo hilo, huku akiweka wazi kuwa kijiji cha Oldonyowas pekee kimepata jumala ya shilingi milioni 747.7.

"Wananchi wamenufaika sana na miradi inayotekelezwa na TASAF, kwaa kuwa hali ya umaskini uliokithiri, imeaanza kupungua na kujidhihirisha katika kijiji chetu, watoto wetu wanaendelea na masomo ya sekondari, wananchi wanafanya ufugaji wa biashara kupitia mradi wa ufuaga kuku chotara, wapo wananchi wanaonufaika na mpango wa kuhawilisha fedha, umasikini unaondoaka Oldonyowas"  amesisitiza Mwenywkiti huyo

Hata hivyo Mwenyekiti huyo wa kijiji, ameweka wazi kuwa, kijiji cha Oldonyowas pekee kimetekeleza jumla ya miradi sita yenye thamani ya shilingi milioni 747.7, na kufafanua kuwa shilingi milioni 34 zimetekelza mradi wa ufugaji kuku chotara, ujenzi wa madarasa na matundu ya vyoo ulioghatimu shilingi milioni 97.8, milioni 76.7 ujenzi wa nyumba za walimu, milioni 104 ujenzi wa jengo la Utawala, ujenzi wa mabweni mawili ya wasichana milioni 175.1, na ujenzi wa mabweni mawili ya wavulana utakaoghatimu shilingi milioni 338.7 Kwa TASAFU awmu ya IV.

ARUSHA DC

KaziIendelee✍✍✍

Mkurugenzi wa OPEC FUND, Dkt. Abdulhamid Khalifa, akiwa na Makamu Mwenyekiti, halmashauri ya Arusha, Mhe. Freddy Lukumai, mbele ya moja ya nyumba za walimu zilizojengwa kwa na TASAF kwa ufadhili wa OPEC FUND, shule ya sekondari Oldonyowas



Mkurugenzi wa OPEC FUND, Dkt. Abdulhamid Khalifa, akikagua moja ya majengo ya nyumba za walimu zilizojengwa kwa na TASAF kwa ufadhili wa OPEC FUND, shule ya sekondari Oldonyowas



Mkurugenzi wa OPEC FUND, Dkt. Abdulhamid Khalifa, akikagua Bweni la wasichana, lililojengwa kwa na TASAF kwa ufadhili wa OPEC FUND, shule ya sekondari Oldonyowas.



Mkurugenzi wa OPEC FUND, Dkt. Abdulhamid Khalifa, akiotesha mti mbele ya Bweni la wasichana, lililojengwa kwa na TASAF kwa ufadhili wa OPEC FUND, shule ya sekondari Oldonyowas.


Picha ya pamoja kati ya Mkurugenzi wa OPEC FUND, Dkt. Abdulhamid Khalifa, walimu, wanafunzi na wananchi, wakiwa mbele ya Jengo la Utawala, lililojengwa kwa na TASAF kwa ufadhili wa OPEC FUND, shule ya sekondari Oldonyowas.



Mkurugenzi wa OPEC FUND, Dkt. Abdulhamid Khalifa, akiwa na wanafunzi wa  shule ya sekondari Oldonyowas.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.