Na. Elinipa Lupembe.
Mfuko wa Maendeleo ya Jamii - TASAF kupitia mradi wa mpango wa kunusuru kaya Masikini, unaendelea kuzinufaisha kaya hizo, kwa kutoa ajira za muda kupitia miradi iliyoibiliwa na kaya hizo na kutekelezwa katika maeneo yao.
Kijiji cha Moivo, kata ya Moivo ni miongoni mwa vijiji 88 vya halmasahauri ya Arusha, vinavyonufaika na mpango huo unaotekelezwa na TASAF awamu ya III, kikiwa na walengwa 250.
Akizungumza kwenye eneo la ujenzi wa kivuko hicho, mwenyekiti wa kamati ya Ujenzi Brazard Mkwizu, amesema kuwa mradi wa ujenzi wa kivuko uliibuliwa na walengwa hao, kutokana na adha kubwa waliyokuwa wakiipata wananchi wa eneo hilo kwa kukosekana kivuko, na kuwasilishwa halmashauri, hatimaye TASAF.
Mkwizu ameweka wazi kuwa eneo hilo lilikiwa ni eneo hatarishi kwa wananchi wa Moivo, nyakati zote za mwaka, huku wahalifu wakitumia eneo hilo kukaba na kunyang'anya watu mali zai, wengine kubakwa huku wengine wakinusurika kuuwawa.
Hata hivyo wanufaika hao wamethibitisha kuwa licha ya TASAF kutatua changamoto ya kivuko katika eneo lao, lakini walengwa hao wamekuwa wakifanya kazi za muda na kulipwa ujira, pesa ambayo huwasaidia kujikimu kimaisha.
"Tunaishukuru serikali kwa kutujengea kivuko, kwa kuwa eneo hili lilikiwa ni hatari hasa nyakati za usiku na alfajiri, vibaka waligeuza kichaka cha wanyang'anyi, tunategemea tatizo hili litakwisha, lakini zaidi sisi walengwa tumepata ajira za muda licha ya kuwa pesa si nyingi sana ila sio sawa na kukosa kabisa, tunafanya kazi kwa moyo kwa kuwa kivuko hiki, kitatusaidia wakazi wote wa Moivo". Amesema Tatu Hamisi mnufaika wa mpango wa Kunusuru kaya Masikini
Naye mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Arusha, Seleman Msumi, amewataka wananchi hao kujitoa kwa moyo wakati wote wa ujenzi mpaka kukamilika kwa kivuko hicho, na akiwasisitiza kukitunza mara baada ya kukamilika.
"Mnapaswa kutambua namna serikali inawathamini na kutatua kero iliyokuwa inawkabili, rai yangu ni kutunza miundo mbinu ya kivuko hiki kwa kiwa serikali intumia fedha nyingi katika kutekeleza miradi, wananchi mnapaswa kuithamini miradi yote" amesisitiza Msumi.
Awali TASAF imetoa kiasi cha shilingi milioni 76 kwa ajili ya utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa Kivuko, huku shilingi milioni 38 zikitumika katika ujenzi na milioni 38 zikitumika kulipa ujira kwa wanakaya walio kwenye mpango wa kunusuru kaya masikini katika kijiji hicho cha Moivo, kwa kufanya kazi za muda kwa masaa na kwa zamu kila siku.
ARUSHA DC
KaziIendelee✍✍
PICHA ZA WANUFAIKA WAKIFANYA KAZI WAKATI WA UJENZI WA KIVUKO MOIVO.
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.