Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha amepokea kibali cha kutekeleza Ikama na Bajeti kwa Ajira Mpya kwa mwaka wa fedha 2022/2023 chenye Kumb.Na.FA.971/288/01/’TEMP’/06 cha tarehe 06 April, 2022 kutoka kwa Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora.
Hivyo, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha anawatangazia wananchi wote ambao ni Raia wa Tanzania wenye sifa kuomba nafasi zilizoorodheshwa hapa chini: -
DEREVA DARAJA LA II – NAFASI 2 - TGS B
SIFA ZA MWOMBAJI
Awe amefaulu kidato cha nne (iv) au cha sita (vi).
Leseni ya daraja E au C ya Uendeshaji magari ambayo amefanyia kazi kwa muda usiopungua mwaka mmoja (1) bila kusababisha ajali.
Awe amehudhuria mafunzo ya msingi ya uendeshaji wa magari (Basic Driving Course) yanayotolewa na Chuo cha mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) au Chuo kingine kinachotambuliwa na Serikali.
Waombaji wenye cheti cha majaribio ya Ufundi Daraja la II watafikiriwa kwanza.
MAJUKUMU YA KAZI YA UDEREVA:
Kukagua gari kabla na baada ya safari ili kubaini hali ya usalama wa gari.
Kuwapeleka watumishi maeneo mbalimbali kwenye safari za kikazi.
Kufanya matengenezo madogo madogo ya gari.
Kukusanya na kusambaza nyaraka mbalimbali,
Kujaza na kutunza taarifa za safari zote katika daftari la safari.
Kufanya usafi wa gari na;
Kufanya kazi nyingine kadri utakavyoelezwa na Msimamizi wa kazi.
MWANDISHI MWENDESHA OFISI DARAJA III (NAFASI 2): - TGS C
SIFA ZA MWOMBAJI:
Awe amefaulu kidato cha nne (IV)
Awe amehudhuria mafunzo ya Uhazili na kufaulu ngazi ya Stashahada (Diploma) kutoka Chuo cha Utumishi wa Umma au Chuo chochote kinachotambuliwa na Serikali.
Awe amefaulu somo la hati mkato ya Kiswahili na Kiingereza, maneno yasiyopungua 80 kwa dakika moja.
Awe na cheti cha programu ya windows, Microsoft office, Internat-E-mail na Publisher, Power point kutoka Chuo kinachotambulika na Serikali.
KAZI NA MAJUKUMU MWANDISHI MWENDESHA OFISI DARAJA III
Kuchapa barua taarifa na nyaraka za kawaida na SIRI.
Kupokea wageni na kuwasaidia shida zao na kuwaelekeza sehemu wanapoweza kushughulikia.
Kutunza taarifa za kumbukumbu za matukio, miadi, wageni, tarehe za vikao, safari za Mkuu wako na ratiba ya kazi nyingine.
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.