AFISA MWANDIKISHAJI JIMBO LA ARUMERU MAGHARIBI AKUTANA NA VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA.
Kuelekea awamu ya pili ya zoezi la uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura na kuweka wazi daftari la awali,leo
May 08,2025 Afisa mwandikishaji Jimbo la Arumeru Magharibi Ndg.Seleman Msumi, amekutana na viongozi wa vyama vya siasa katika kikao kilicholenga kuwapa taarifa muhimu kuhusu awamu ya pili ya zoezi la uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura.
Msumi alitumia fursa hiyo kuwahimiza viongozi hao kuandaa mawakala ambao watashiriki kusimamia zoezi hilo katika vituo kwa kufuata kanuni na taratibu zilizowekwa na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC).
Aidha kuwahamasisha wananchi wote wanaoguswa na zoezi hilo kujitokeza ili waweze kupata fursa yakushiriki Uchaguzi mkuu wa Oktoba 2025.
Vyama vya siasa ni wadau muhimu katika mchakato mzima wa uchaguzi unaohusisha uandikishaji wa wapiga kura wapya pamoja na uboreshaji wa taarifa za awali katika daftari la kudumu la wapiga kura.
Awamu ya pili ya uboreshaji Jimbo la Arumeru Magharibi itafanyika kwa siku saba kuanzia Mei 16 - 22 ,2025 kwenye vituo 42 vilivyoanishwa kwenye kata zote 27 za Halmashauri ya Wilaya ya Arusha.
"Kujiandikisha kuwa mpiga kura ni msingi wa uchaguzi bora".
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.