Halmashauri ya Arusha, imeanza rasmi kutekeleza kwa vitendo mradi wa ujenzi wa kituo kipya cha afya Matevesi, kufuatia maagizo yaliyotolewa na serikali kupitia Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, kwa halmasahuri zote nchini kutumia mapato ya ndani kujenga kituo cha afya.
Mkurugenzi Mtendaji, halmashauri ya Arusha, Seleman Msumi, amesema kuwa, halmashauri yake, imeanza rasmi ujenzi wa kituo kipya cha afya katika kata ya Matevesi, ikiwa ni utekelezaji wa maagizo ya Mheshimiwa Waziri, Ofisi ya Rais TAMISEMI, maagizo yaliyoelekeza kila halmasahuri kutumia shilingi milioni 500 ya mapato ya ndani kwa mwaka wa fedha 2021/2022, kujenga kituo cha afya kwa kata ambazo hazina vituo vya afya.
Mkurugenzi Msumi, ameweka wazi kuwa, halmashauri imeanza kutekeleza awamu ya kwanza ya mradi wa ujenzi wa kituo hicho cha afya Mateves, kwa kujenga jengo la wagonjwa wa nje (POD), mradi utakaogharimu kiasi cha shilingi milioni 310.
Naye Afisa Mipango, halmashauri ya Arusha,Anna Urio, amefafanua kuwa, kukamilika kwa mradi huo wa ujenzi wa kituo cha afya Mateves, utagharimu kiasi cha shilingi milioni 500, ambapo kwa wamu ya kwanza umeanza ujenzi wa jengo la wagonjwa wa nje.
Katika mwaka wa fedha 2021/2022, halmashauri ya Arusha imefanikisha ujenzi wa vituo vitatu vya afya, ikiwemo kituo kipya cha Afya cha Mwandet, kinachojenhwa kwa fedha kutoka serikali kuu, huku vituo viwili vikijengwa kwa mapato ya ndani, kituo kipya cha afya cha Oloirieni na kituo kipya Mateves vyote vikijengwa kwa fedha za mapato ya ndani.
ARUSHA DC
KaziInaendelea✍✍
Mkurugenzi Mtendaji, halmashauri ya Arusha, Seleman Msumi, akikagua maendeleo ya ujenzi wa Kituo kipya cha Afya Mateves, mradi unaotekelezwa kwa fedha za mapatao ya ndani ya halmashaurinhiyo.
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.