• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

ARUSHA DC YAJIPANGA KUWABANA WAZAZI WASIOTOA CHAKULA CHA WATOTO WAO SHULE ZA KUTWA...

Posted on: May 19th, 2023

Na Elinipa Lupembe

Katika kukabiliana na changamoto ya baadhi ya watoto kutokupata chakula cha mchana wawapo shuleni kwa shule za kutwa, halmashauri ya Arusha imeandaa sheria ndogo za kuwabana wazazi wasiotoa chakula kwa ajili ya watoto wao.

Hayo yamewekwa wazi wakati wa kikao cha kamati ya Lishe cha kujadili taarifa za Lishe za halmashauri hiyo kwa kipindi cha robo ya tatu ya kuanzia mwezi Januari - Machi 2023, kikao kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa halmashauri hiyo.


Katika kikao hicho Idara mtambuka za Elimu, Kilimo, Afya, Maendeleo ya Jamii na Mipango ziliwasilisha taarifa za utekelezaji wa shughuli za Lishe kwa kipindi cha robo hiyo ya tatu kiseta, huku taarifa Idara za Elimu Msingi na Sekondari zikionyesha bado kuna changamoto ya baadhi ya wanafunzi kutokupata chakula cha mchana kwa shule za kutwa.

Akitoa ufafanuzi wa taaifa hiyo Afisa Elimu Sayansi Kimu shule za Msingi, Mwl. Boniface Mwang'onda amesema kuwa licha ya juhudi kubwa ya uhamasishaji na utoaji wa wa elimu kwa jamii na wazazi, kati ya wanafunzi 77,574 wa shule 100 za msingi za serikali wanafunzi 51,125 tu ndio hupata chakula cha mchana shuleni na wanafunzi 26,446 hawapati chakula cha mchana sawa na 34%.


Hata hivyo, Mwanasheria na Wakili Msomi Eliasifiwe Kileo, ameweka wazi kuwa, tayari halmashauri imeandaa sheria ndogo, zitakazotumika kuwabana wazazi ambao hawatatoa chakula cha mchana kwa watoto wao wanaosoma shule za kutwa kwa kuzingatia sheria mama ya sera ya elimu ya mwaka 2014 pamoja na taratibu na makubaliano waliyojiwekea wazazi wenyewe kupitia kamati za shule husika.

"Tayari mchakato wa Sheria ndogo za halmashauri umekamilika na kupitishwa na Baraza la Waheshimiwa Madiwani, kwenda ngazi ya mkoa na kusainiwa na Ofisi ya Rais TAMISEMI na hatimaye kuanza kutumika rasmi, sheria ambayo itatoa nafasi ya mzazi kushitakiwa Mahakamani kwa kosa la kukaidi kumlipia mtoto wake chakula cha mchana awapo shuleni". Amefafanua Wakili huyo Msomi.

Naye mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha, amewataka wazazi kutambua umuhimu wa watoto wao kupata chakula cha mchana wawapo shuleni kwa kuzingatia uhusiano mkubwa wa lishe na taaluma yaani tendo la kujifunza.

"Wazazi hakikisheni watoto wenu wanapata chakula cha mchana wawapo shuleni kwa kuwa ni haki yao ya msingi lakini zaidi kushindwa kufanya hivyo ni ukatili unaoathiri hali ya ujifunzaji kwa mtoto na hudhoofisha uelewa na ufaulu huku ikishusha kiwango cha taaluma shuleni, wazazi watendeeni haki watoto wenu, msisubiri kubanwa na sheria". Amesema Msumi.

Hata hivyo Afisa Lishe halmashauri ya Arusha, Doto Milembe ameeleza kuwa lishe bora huwezesha makuzi ya mwili na akili ya mtoto, na hujenga ubongo wa mtoto na kuchangamsha akili ya mtoto itakayomrahisishia uelewa wa haraka wakati wa kujifunza.

"Jamii inapaswa kutambua suala la lishe kwa mtoto si suala la serikali bali ni wajibu wa mzazi kumpatia mtoto wake chakula bora, kitakachojenga mwili na akili yake na kumpa mtoto uwezo wa kujifunza kwa urahisi, lishe duni husababisha udumavu wa mwili na akili" Amesisitiza Afisa Lishe huyo.

Serikali imebainisha wazi wajibu wa wazazi wa kuwapa chakula cha mchana watoto wao kwa shule za kutwa kupitia Sera ya Elimu ya mwaka 2014 na Sheria ya Kimataifa ya mtoto namba 22 na mwongozo wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia ya mwaka 2022 inayosisitiza wazazi kutoa chakula cha mchana kwa mtoto nyumbani na shuleni ikiwa ni haki yake ya msingi.


ARUSHA DC ni Yetu, Tushirikiane Kuijenga"

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.