Na. Elinipa Lupembe.
Halmashauri ya Arusha, imepokea gari kutoka serikalini kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii - TASAF 'Toyota Land Cruser' lenye namba za usaji STM 0594, kwa ajili ya ufuatiliji wa utekelezaji wa miradi ya TASAF.
Mkurugenzi Mtendaji, halmashauri ya Arusha, Seleman Msumi, ameishukuru Serikali ya awamu ya sita, inayoongozwa na Mama Samia Suluhu Hassan, kwa kwapatia gari kwa ajili ya kufuatilia miradi inyotekelezwa na TASAF katika halmashauri hiyo.
Mkurugenzi Msumi amemshukuru mheshimiwa Rais, kwa kuona umuhimu wa halmashauri kuwa na magari kwa ajalili ya miradi ya TASAF, huku akithibitisha kuwa gari hilo litarahisisha ufuatiliaji wa miradi inayotekelezwa na TASAF katika vijiji 88, vya halmashauri ya Arusha, vinavotekeleza miradi hiyo ya TASAF.
"Kwa Jiografia ya halmashauri ya Arusha, kuna maeneo ambayo hayafikiki kirahisi kwa magari ya kawaida, ila uwepo wa gari hili utawarahisishia watalam kuifikia miradi na walengwa kwa urahisi na kwa wakati, jambo ambalo litawezesha halmashauri kufikia malengo yaliyokusudiwa na serikali, hususani kwenye miradi ya kaya zenye uhitaji zinazohudumiwa na TASAF". Amesistiza Mkurgenzi Msumi.
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.