• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

ARUSHA DC YAPOKEA VIFAA VYA MILIONI 16.6 KUJIKINGA NA CORONA

Posted on: May 24th, 2020

Na. Elinipa Lupembe

Halmashauri ya Arusha imepokea vifaa vyenye thamani ya shilingi milioni 16.6 , kutoka kwenye Asas ya kiraia ya Kilmanjaro Technology Foundation, kwa ajili ya kujinga na kupambana na ugonjwa wa Corona unaosababishwa na virus vya Covid 19.

Akikabidhi vifaa hivyo, kwenye ofisi za makao makuu ya halmashauri hiyo, mwishoni mwa wiki iliyopita, Meneja wa Kilimanjaro Technology Foundation, Lidya Maliti, amesema kuwa, shirika limeamua kuunga mkono juhudi za serikali ya awamu ya tano za kupambana na gonjwa la hatari la Corona kwa kutoa vifaa hivyo, vitumike kwenye taasisi za Umma, kwa lengo la kujikinga na gonjwa hilo.

"Ugonjwa wa Corona upo, inatubidi tuishi nao kwa kuchukua tahadhari kwa kunawa mikono kwa maji tiririka na sabuni katika maeneo yetu ya kazi, huku tukiendelea kuchapa kazi na kulijenga taifa letu, kama mheshimiwa Rais wetu alivyoelekeza" amesema Meneja huyo

Imeelezwa kuwa vifaa vilivyotolewa vina thamani ya shilingi milioni 16.6, ikiwa ni pamoja na Ndoo 1000 za kunawia mikono, Barakoa 1000 za vitambaa kwa ajili ya watumishi wa Umma na Barakoa nyingine 1,000 'surgical mask' kwa ajili ya wahudumu wa afya.

Meneja Lidya ameelekeza vifaa hivyo kugawiwa kwenye ofisi za  taasisi za Umma, ndani ya halmashauri hiyo, ikiwemo ofisi  za makao makuu, ofisi za kata na vijiji, masoko na minada, vituo vya afya na zahanati zote, shule za msingi na sekondari, Mahakama, kituo cha Polisi vilivyopo kwenye halmashauri ya Arusha.

Naye Kaimu Mkurugenzi Halmashauri ya Arusha, Paulus Kessy, mbali na kuishukuru ASAS hiyo kwa msaada huo, ameeleza kuwa, vifaa hivyo vimekuja wakati muafaka ambapo, wananchi wameruhusiwa kuendelea na shughuli zao za kila siku huku wakitakiwa kuendelea kuchukua tahadhari ya gonjwa hatari la Corona, kwa kunawa mikono mara kwa mara, kuvaa barakoa pamoja na kutumia vitasa mikono.

Aidha Kaimu mkurugenzi huyo, amewataka wananchi kuendelea kutekeleza majukumu yao kwa kufanyakazi kwa bidii, sambamba na kuchukua tahadhali kwa kujikinga na gonjwa la Corona, zaidi  kufuata maelekezo ya Serikali na yanayotolewa na watalamu wa Afya.

Msimamizi wa Ofisi, halmashauri ya Arusha, Grace Mburuja, amesema kuwa, vifaa hivyo ni muhimu kwa watumishi wa taasisi za serikali kwani wao, huwahudumia wananchi wengi kutoka maeneo tofauti, kupitia vifaa hivyo watumishi watafanyakazi kwa uhuru bila hofu ya kupata maambukizi ya Corona.

Uongozi wa halmashauri ya Arusha, unawahimiza wananchi wote, kuendelea kuchukua tahadhari ya gonjwa la Coron kwa kunawa mikono, kutumia vitakasa mikono 'sanitizer' na kuvaa Barakoa wakati wote wakiwa kazini hasa kwenye mikusanyiko.

Kaimu mkurugenzi halmashauri ya Arusha, Paulus Kessy akipokea ndoo ya kunawia mikono kutoka kwa Meneja wa Asas ya kiraia ya Kilimanjaro Technology Foundation Lidya Maliti.


Kaimu mkurugenzi halmashauri ya Arusha, Paulus Kessy akipokea barakoa tiba 'surgical mask' kwa ajili ya wahudumu wa afya wa halmashauri hiyo, kutoka kwa Meneja wa Asas ya kiraia ya Kilimanjaro Technology Foundation Lidya Maliti, kulia ni Afisa Elimu Msing, mwalimu Hossein Mghewa.

Kaimu mkurugenzi halmashauri ya Arusha, Paulus Kessy akipokea barakoa za kitambaa kwa ajili ya watumishi wa Umma wa halmashauri hiyo, kutoka kwa Meneja wa Asas ya kiraia ya Kilimanjaro Technology Foundation Lidya Maliti.


Mganga Mkuu, halmashauri ya Arusha, Dkt. Petro Mbaya,akiwa na barakoa tiba 'surgical mask' kwa ajili ya wahudumu wa afya wa halmashauri hiyo, tayari kwa kwenda kuanza kuanza kazi ya kuwahudumia wagonjwa.



Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.