Halmashauri ya Arusha wilaya ya Arumeru imeibuka kidedea na kuwa mshindi wa kwanza kwenye sekta ya Kilimo na Mifungo, katika maonesho ya Wakulima Nanenane, Kanda ya Kaskazini kwa kufanikiwa kuzibwaga halmashauri 20 za mikoa mitatu ya Arusha, Kilimanjaro na Manyara.
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mheshimiwa Abdallah Ulega, amekabidhi MAKOMBE MAWILI kwa halmashauri ya Arusha wakati akihitimisha maonesho ya Wakulima 2020, Kanda ya Kaskazini yaliyofanyika kwenye viwanja vya Themi Jijini Arusha.
Halmashauri hiyo imefanikiwa kuwa mshindi wa kwanza kwenye mashindano ya Mazao na Mshindi wa kwanza pia kwenye mashindano ya Mifugo na kufanikiwa kupata Makombe mawili ya Mazao na Mifugo.
Hata hivyo watalamu wa halmashauri hiyo, wameweka wazi kuwa, siri kubwa ya ushindi ni ushirikiano mkubwa wa timu ya menejimenti ya halmashauri hiyo, ikiongozwa na mkurugenzi mtendaji, kazi kubwa inayofanywa na watalamu wa kilimo na mifugo kwa kuhamishia ofisi shambani waliko wakulima na sio kukaa ofisini peke.
Hongera sana Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha Saad Mtambule, hongera sana Watalamu wa Kilimo na Mifugo, hongera sana Menejimenti na watalamu wote sambamba na timu ya ushindi ya Halmashauri ya Arusha, hongera nyingi sana kwa Wakulima na Wafugaji wote wa halmashauri ya Arusha, hongera nyingi mnoo kwa wananachi wote wa halmashauri ya Arusha.
Team work spirit is our core value....
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.