Na. Elinipa Lupembe.
Katika kutekeleza mkakati wa kuboresha miundombinu ya shule, serikali kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii -TASAF, imewakumbuka wavulana wa shule ya sekondari Oldonyowas, kwa kutoa fedha kwa ijali ya utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa mabweni mawili ya wavulana shule ya sekondari Oldonywas, halmashauri ya Arusha, baada ya kujenga mabweni mawili ya wasichana shuleni hapo.
Akizungumza wakati wa kukagua maendeleo ya utekelezaji wa mradi huo, mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha, Seleman Msumi, ameweka wazi kuwa, kwa mara nyingine tena, serikali kupitia mfuko wa TASAF imetoa fedha, kiasi cha shilingi milioni 320, kwa ajili ya ujenzi wa mabweni mawili ya kulala wanafunzi wavulana 160, shule ya sekondari Oldonyowas, hii ni baada ya awamu ya kwanza kujenga mabweni mengine mawili ya wasichana kwa shule hiyo.
Mkurugenzi Msumi amethibitisha umuhimu wa shule hiyo kuwa na mabweni kwa wanafunzi wa jinsi zote, ni kutokana na asili ya mazingira ya eneo hilo, watoto wengi wanaishi mbali na shule na kusababisha kitembea umbali mrefu kwenda na kurudi shuleni, jambo ambalo linawaathiri kiafya, kisaikolojia na hata kitaaluma.
"Ninampongeza Rais wetu, Mama Samia kwa kusikia kilio cha watoto wake, watoto wa Oldonyowas, na kujenga mabweni ya wavulana pia, tunaamini uwepo wa mabweni utaongeza ari ya wanafunzi kupenda shule, kutapunguza watoto kuacha shule, kwa kuwa na mazingira tulivu ya kujisomea, jambo ambalo litapandisha taaluma shuleni na kuongeza kiwango ya ufaulu kwa wanafunzi " Amefafanua Mkurugenzi Msumi
Naye Michael Ismail mwanafunzi wa kidato cha nne, licha ya kuishukuru serikali ya awamu ya sita, amefurahishwa na kitendo cha kujengwa mabweni ya wavulana shuleni hapo, ambapo awali kulikuwa na mabweni ya wasichana peke yao na kuongeza kuwa wanafunzi wengi hukosa muda wa kujisomea wawapo nyumbani, kutokana na uchovu wa kutembea umbali mrefu, huku wazazi wakiwapangia majukumu ya kazi za nyumbani mara watokapo shuleni.
"Watoto wengi wanaishi mbali na shule lakini wakifika nyumba watapewa kazi za kuchunga ama kukata majani ya mifungo, jambo ambalo linatukosesha muda wa kujisomea hasa tuwapo nyumbani, lakini tukiwa na mabweni itatusaidia kutumia muda mwingi kujisomea kwa pamoja na kuturahisishia kufanya kazi za shule kwa kujadiliana katika makundi 'group discussion'". amefafanua mwanafunzi Michael
Mradi huo wa ujenzi wa mabweni mawili ya wavulana shule ya sekondari Oldonyowas, unafanya kuwa na idadi ya miradi tisa tofauti iliyotekelezwa na TASAF katika shule hiyo, ikiwemo vyumba vya madarasa, mabweni mawili ya wasichana, jengo la utawala, matundu ya vyoo, nyumba za walimu.
ARUSHA DC
KaziInaendelea✍✍✍✍
JIANDAE KUHESABIWA 23.08.2022
Mkurugenzi Mtendaji, halmashauri ya Arusha, Seleman Msumi (wa kwanza kushoto)akisikiliza maelezo kutoka kwa Msimamizi wa mradi wa ujenzi wa mabweni ya wavulana shule ya sekondari Oldonyowas, QS. Bibie Manzi ( wa kwanza kulia)
Mkurugenzi Mtendaji, halmashauri ya Arusha, Seleman Msumi akiwangoza wakuu wa Idara na vitengo kukagua maendeleo ya utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa mabweni ya wavulana shule ya sekondari Oldonyowas.
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.