• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

BADALA YA KUOTESHA MAUA OTESHA MBOGA KWA LISHE BORA YA FAMILIA

Posted on: August 8th, 2022

Na Elinipa Lupembe.

Kufuatia changamoto ya ufinyu wa maeneo  kwa wakazi wa halmashauri ya Arusha hususani ukanda wa Juu, wametakiwa kufanya kilimo cha nyumbani kwa kutumia mifuko kuotesha mbogamboga kwa matumizi ya nyumbani na biashara pia.

Rai hiyo imetolewa na watalamu wa kilimo wakati wa maonyesho ya Nanenane kanda ya Kaskazini, teknolojia inayopatikana kwenye banda la kilimo, halmashauri ya Arusha, maonyesho yanayoendelea kwenye viwanja vya Themi -Njiro Jijini Arusha.

Afisa Kilimo mboga mboga, halmashauri ya Arusha, Lucy Mvungi amebainisha kuwa, kutokana na ufinyu wa maeneo katika halmashauri hiyo, hususani kwenye ukanda wa juu, wananchi wanatakiwa kutumia teknolojia ya Kilimo cha Nyumbani cha kuotesha mazao ya mbogamboga kwenye mifuko, ambayo ikioteshwa na kutunzwa vizuri ina muonekano mzuri unaovutia kama ule wa maua nje ya nyumba.

Bi Kilimo huyo, amewashauri wananchi, badala ya kuotesha maua mengi kuzunguka nyumba, ni vema wakaotesha mboga za aina mbalimbalo katika neo hilo dogo, ili kupata chakula kitakachokidhi mahitaji ya familia, sambamba na kuipatia familia lishe bora.

"Unapokuwa na bustani ya mbogamboga nyumbani, inakupunguzia gharama za kununua mboga kila siku, lakini inaipa familia yako uhakika wa kuwa na afya bora, kutokana na uhakika wa upatikanaji wa lishe bora inayotokana na mboga za majani". Amefafanua Afisa Kilimo Lucy.

Aidha ameongeza kuwa kilimo hicho ni rahisi, na hakichukui muda mrefu na kusisitiza kuwa mfuko huo wa sulfeti ukitunzwa vizuri una uwezo wa kudumu zaidi ya miaka miwili na mboga zake hukaa miezi 6 mpaka miaka 2 kutegemea aina ya mboga zilizooteshwa.

Amezitaja aina za mbogamboga zinazoweza kuoteshwa kwenye mifuko ni pamoja na spinachi, saladi, sukuma wiki, bitruti, nyanya chungu, mnafu, saro, nyanya, pilipili kali na pilipili hoho.

Karibu banda la Kilimo halmashauri ya Arusha, kujionea teknolojia mbalimbali za kilimo cha kisasa, ikiwemo kilimo cha nyumbani, uchaguzi wa mbegu bora, upatikanaji wa oembejeo za kilimo na mikopo ya matrekta kwa wakulima kuelekea Ajenda 10 -30 Kilimo Biashara.

KAULI MBIU: "AJENDA  10 -30 KILIMO NI BIASHARA 'SHIRIKI KUHESABIWA KWA MIPANGO BORA YA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI"


PICHA ZA SHAMBA LA NYUMBANI

Banda la Kilimo halmsahuri ya Arusha likiwa limepambwa na bustani nzuri ya mbogamboga zilizooteshwa kwanye mifuko, 



Mboga mboga zilizooteshwa kwenye mifuko, kilimo kinachoshauriwa kufanyika nyumbani kwenye eneo dogo



Matangazo

  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI WA ROBO YA TATU 2O21/2022 tarehe 09.05.2022 May 08, 2022
  • Tazama zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI WA ARUSHA DC,BW.SELEMAN MSUMI AKIWA NA WATUMISHI WA HALMASHAURI HIYO KATIKA MASDHIMISHO YA MEI MOSI KIMKOA ARUSHA

    May 02, 2025
  • HERI YA MEI MOSI

    May 01, 2025
  • HERI YA SIKU YA MEI MOSI

    May 01, 2025
  • MHE. MAJALIWA MGENI RASMI KATIKA MAADHIMISHO YA SIKU YA UHURU WA VYOMBO VYA HABARI DUNIANI

    April 29, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.