Baraza la madiwani Halmashauri ya Arusha wameridhishwa na utekelezaji wa miradi ndani ya katika Kata zote 27 pongezi zilizotolewa kupitia kikao cha robo mwaka kwa mwaka wa fedha 2024/2025.
Akiongea katika kikao cha Baraza la Madiwani, Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo ya Wilaya ya Arusha Dkt.Ojungu Salekwa alisema kuwa kazi kubwa ya Halmashauri ni kuhakikisha inatekeleza mahitaji muhimu kwa wanawanchi.
"Kwakweli niseme kuwa licha ya kuwepo kwa changamoto za hapa na pale na hasa katika kipindi hiki Cha mvua lakini Halmashauri yetu kupitia ofisi ya mkurugenzi imejitahidi kufanikisha kwa kiasi kikubwa baadhi ya miradi kwenye kata zetu" Alisema Dkt.Ojungu.
Aidha Dkt Ojungu aliongeza kuwa hoja kubwa iliyoibuliwa kwenye Baraza ni hoja ya miundombinu ya Barabara ambayo imeonekana kuwa kero kwenye baadhi ya Kata katika Halmashauri, hivyo Halmashauri imekusudia kuanza kupanga fedha kwa kushirikiana na TARURA Ili kuweza kukarabati baadhi ya miundombinu ambayo imebainika kuwa hatalishi kwa wananchi.
Kwa upande wake diwani wa kata ya Oltroto ambaye pia ni mwenyekiti wa kamati ya huduma za jamii Elimu,Afya na maji pamoja na miundombinu,Mhe. Baraka Simon alisema kuwa Baraza limeelekeza mambo muhimu hasa ya utatuzi wa changamoto ikiwemo ujenzi wa madarasa, na barabara kwenye kata hasa kwenye kipindi hiki cha mvua na kwahiyo million 40.5 zitatolewa na Halmashauri kwa ajili ya utatuzi wa changamoto hiyo.
Sambamba na Hilo mhe.Baraka ameipongeza ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha ndugu Suleiman Msumi kwa kuweza kufikia malengo ya makadirio ya makusanyo ya mapato ndani ya Halmashauri kiasia cha bilioni 6.9 na kuweza kukusanya kiasi cha bilioni 5.01 hadi kufikia kipindi cha robo tatu ya mwaka wa fedha 2024/2025.
Naye Mkurugenzi Halmashauri ya Arusha Ndugu Suleiman Msumi amewashukuru wajumbe wa Baraza la madiwani kwa kuonyesha ushirikiano wao kipindi chote Cha uongozi wake tangia ateuliwe kuiongoza Halmashauri hiyo.
"Kwakweli kwa heshima ya pekee nitoe shukrani zangu kwenu nyote kwa jinsi mlivyo onyesha ushirikiano wenu kwangu na kwa wataalam wangu, mafanikio ambayo tumeendelea kuyapata Halmashauri ya wilaya ya Arusha yametokana na utayari wenu wa kujitoa.
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.