• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

BARAZA LA WAFANYAKAZI ARUSHA DC LAJADILI NA KUPITISHA BAJETI YA 2025/2026

Posted on: January 28th, 2025

BARAZA LA WAFANYAKAZI ARUSHA DC LAJADILI NA KUPITISHA BAJETI YA 2025/2026
Baraza la Wafanyakazi la Halmashauri ya Wilaya ya Arusha limejadili na kupitisha mapendekezo ya Bajeti ya Mapato na Matumizi ya shilingi bilioni 68.1 kwa mwaka wa fedha 2025/2026, katika kikao maalum kilichofanyika ukumbi wa Halmashauri hiyo mkoani Arusha.
Akizungumza wakati wa kikao hicho, Mwenyekiti wa kikao ambaye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha, Bw. Seleman H. Msumi, alieleza kuwa kila mfanyakazi ana jukumu la kutimiza wajibu wake kwa kushirikiana ili kufanikisha malengo ya maendeleo ya Halmashauri hiyo. Alisisitiza kuwa ushirikiano na utekelezaji wa majukumu kwa kuzingatia Bajeti iliyopitishwa ni hatua muhimu ya kufanikisha adhima ya Halmashauri.
“Ni jukumu letu kuhakikisha tunazingatia sheria, taratibu, na miongozo katika kutekeleza majukumu yetu. Kila mmoja wetu ahakikishe anatimiza wajibu wake kwa bidii kwa ajili ya maendeleo ya wananchi,” alisema Bw. Msumi.
Awali, akiwasilisha rasimu ya Bajeti hiyo, Afisa Mipango na Uratibu wa Halmashauri, Bi. Anna Urio, alifafanua kuwa jumla ya shilingi bilioni 7.2 zinatarajiwa kutoka vyanzo vya mapato ya ndani, shilingi bilioni 48.4 zitatumika kwa mishahara ya watumishi, shilingi bilioni 2.9 kwa ruzuku ya uendeshaji, na shilingi bilioni 9.6 kwa miradi ya maendeleo, fedha zote zikitolewa na Serikali Kuu.
Bi. Urio aliongeza kuwa mapendekezo na maazimio ya kikao hicho yamechukuliwa kwa umakini mkubwa, na ofisi ya Mipango na Uratibu imeahidi kushirikiana na idara mbalimbali ili kuhakikisha utekelezaji wa bajeti hiyo unaleta maendeleo chanya ndani ya Halmashauri.Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali za Mitaa (TALGWU) Halmashauri ya Wilaya ya Arusha, Dkt. Paschal Daniel Kangiria, aliipongeza timu ya uandaaji wa bajeti kwa umakini na weledi waliouonyesha. Aidha, alisifu hatua za Halmashauri hiyo katika kuhakikisha kuwa mapendekezo ya bajeti yamezingatia maslahi ya wafanyakazi na maendeleo ya jamii.

Baraza la Wafanyakazi la Halmashauri ya Wilaya ya Arusha limejadili na kupitisha mapendekezo ya Bajeti ya Mapato na Matumizi ya shilingi bilioni 68.1 kwa mwaka wa fedha 2025/2026, katika kikao maalum kilichofanyika ukumbi wa Halmashauri hiyo mkoani Arusha.


Akizungumza wakati wa kikao hicho, Mwenyekiti wa kikao ambaye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha, Bw. Seleman H. Msumi, alieleza kuwa kila mfanyakazi ana jukumu la kutimiza wajibu wake kwa kushirikiana ili kufanikisha malengo ya maendeleo ya Halmashauri hiyo. Alisisitiza kuwa ushirikiano na utekelezaji wa majukumu kwa kuzingatia Bajeti iliyopitishwa ni hatua muhimu ya kufanikisha adhima ya Halmashauri.


“Ni jukumu letu kuhakikisha tunazingatia sheria, taratibu, na miongozo katika kutekeleza majukumu yetu. Kila mmoja wetu ahakikishe anatimiza wajibu wake kwa bidii kwa ajili ya maendeleo ya wananchi,” alisema Bw. Msumi.


Awali, akiwasilisha rasimu ya Bajeti hiyo, Afisa Mipango na Uratibu wa Halmashauri, Bi. Anna Urio, alifafanua kuwa jumla ya shilingi bilioni 7.2 zinatarajiwa kutoka vyanzo vya mapato ya ndani, shilingi bilioni 48.4 zitatumika kwa mishahara ya watumishi, shilingi bilioni 2.9 kwa ruzuku ya uendeshaji, na shilingi bilioni 9.6 kwa miradi ya maendeleo, fedha zote zikitolewa na Serikali Kuu.


Bi. Urio aliongeza kuwa mapendekezo na maazimio ya kikao hicho yamechukuliwa kwa umakini mkubwa, na ofisi ya Mipango na Uratibu imeahidi kushirikiana na idara mbalimbali ili kuhakikisha utekelezaji wa bajeti hiyo unaleta maendeleo chanya ndani ya Halmashauri.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali za Mitaa (TALGWU) Halmashauri ya Wilaya ya Arusha, Dkt. Paschal Daniel Kangiria, aliipongeza timu ya uandaaji wa bajeti kwa umakini na weledi waliouonyesha. Aidha, alisifu hatua za Halmashauri hiyo katika kuhakikisha kuwa mapendekezo ya bajeti yamezingatia maslahi ya wafanyakazi na maendeleo ya jamii.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.