• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

KONGA LA WAVIU ARUSHA DC LASAIDIA WAATHIRIKA WA VVU KUIMARIKA KIAFYA NA KIUCHUMI

Posted on: December 1st, 2021

Na. Elinipa Lupembe.

Wananchi, Halmashauri ya Arusha wameungana na watu wote duniani, kuadhimisha siku ya UKIMWI Duniani, huku Baraza La watu wanaoishi na virusi vya UKIMWI (WAVIU) halmashauri hiyo, likiwa na mafanikio na matumini makubwa ya kimaisha, kupitia uwezeshwaji unaofanywa kwa ushirikiano  mkubwa kati ya  ASASI za kiraia na halmashauri ya Arusha.

Wakizungumza  wakati wa maadhimisho ya siku ya UKIMWI duniani, yaliyofanyika kwenye viwanja vya Balbal kata ya Oloirieni halmashauri ya Arusha, WAVIU hao wameweka wazi kuwa, kutokana na uwezeshaji kupitia mafunzo mbalimbali ya kiafya, kijamii na kiuchumi, wanayoyapata kupitia Baraza hilo la WAVIU, Baraza limeweza kuwafanya watu wanaoishi na VVU, kujikubali na kujiamini kwa kuacha kujinyanyapaa wenyewe, kuimarika kiafya kwa kutumia ARV kwa ufasaha, kujiinua kiuchumi kupitia shughuli za ujasiriamali zinazofanywa kupitia vikundi vya WAVIU.

Mweka Hazina wa Baraza la WAVIU halmashauri ya Arusha, Trifonia  Mdendemi, amethibitisha kuwa kupitia konga lao la WAVIU, baraza limefanikiwa kuwaunganisha kwenye vikundi takribani waathirika 280 wa VVU, vikundi ambavyo vimejengewa uwezo wa kujikubali, kuacha kujinyanyapaa, kutumia dawa za ARV kwa ufasa na kuwa mabalozi wa kuibua na kuwatia moyo WAVIU ambao wamekata tamaa, jambo ambalo limefanikiwa kwa zaidi ya asilimia 80 kupitia malengo ya mwaka huu wa 2021.

"Mpaka sasa tuna jumla ya vikundi 25 vya wajasiriamali WAVIU 280 katika kata 5, wote wamepata mafunzo ya kuwawezesha  kufanya biashara ndogo ndogo, zinazowaingizia kipato cha familia, na kuziwezesha familia kumudu kupata mahitaji muhimu ya familia, jambo lililorejesha amani na matumaini makubwa kwa WAVIU wengi, tofauti na zamani WAVIU wengi walikata tamaa kwa kutengwa na jamii inayowazunguka na kujiona wao na wakufa tuu" amefafanua Trifonia.

Naye Mgeni rasmi katika maadhimisho hayo,  Mkurugenzi mtendaji halmashauri ya Arusha, Selemani Msumi, amewapongeza WAVIU hao na kuwatia moyo kuendelea kuishi kwa matumaini, huku wakijiamini mbele ya jamii na kufanya kazi zao za uzalishaji mali kwa bidii, kazi ambazo licha ya kuingiza kipato cha familia lakini pia ni msingi wa maendeleo ya jamii na Taifa kwa ujumla.

Ameongeza kuwa, halmashauri itaendela kushirikiana na ASAS za kiraia, kuwaimarisha na kuwajengea uwezo WAVIU hao, pamoja na kuhamasisha jamii, kupambana na maambukizi mapya ya VVU mpaka kufikia asilimia 95 ifikapo 2030, kuondoa unyanyapaa ndani ya jamii, pamoja na kuhakikisha WAVIU hao wanapata dawa za kufubaza makali ya VVU kwa wakati na kwa usahihi, kupitia vituo vyote vya kutolea huduma za afya.

"Nimevutiwa sana na maonesho ya shughuli mbalimbalai za kupambana na UKIMWI kiseta, nendelee kuwatia moyo ndugu zangu, serikali yenu makini iko pamoja na ninyi, kwa kuwa mnazidi kuuthibitishia Umma, kwamba UKIMWI ni ugonjwa kama magonjwa mengine, ugonjwa ambao  ukijikubali na  ukizingatia masharti yanayolelekezwa na wahudumu wa afya, na ukatumia dawa kwa usahihi, unaweza kuishi maisha marefu na kutimiza ndoto zako, tofauti na dhana iliyojengeka hapo awali, kwamba ukipata maambukizi ya VVU wewe ni wa kufa tuu" amesisitiza mkurugenzi huyo.

Naye Mratibu wa UKIMWI halmashauri ya Arusha, Upendo Elisamehe, Lengo la maadhimisho ya siku ya UKIMWI Duniani, ni kitoa fursa ya kutathmini hali na kuhusu uthibiti UKIMWI ambayo husaidi katika kubaini changamoto, mafanikio na kuwa na mkakati katika kupambana na maambukizi ya VVU pamoja na UKIMWI katika jamii zetu. 

"Maadhimisho haya yanafanyika ili kuikumbusha jamiii kuendelea kujikinga dhidi ya maambukizi ya mapya ya VVU na kuwakumbusha watu wenye maambukizi kutumia dawa za kufubaza makali ya VVU kwa ufasaha bili kuacha, kubwa zaidi, jamii kuacha unyanyapaa kwa watu wenye amambukizi na kuwapa huduma stahiki kwa upendo" amesisitiza Mratibu huyo wa UKIMWI.Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani  halmashauri ya Arusha 2021,  yamefanyika kwa ushirikiano wa halmashauri hiyo na mashirika ya ACE Africa, CWCD, Kizazi Kipya, HIMD huku kauli mbiu ikisisistiza 'Zingatia Usawa, Tokomeza UKIMWI, Tokomeza magonjwa ya Mlipuko'.

ARUSHA DC 

#KaziIendelee✍


Mweka Hazina wa Konga la WAVIU halmashauri ya Arusha, Trofina Mdendemi (wa pili kushoto) akimuonyesha na kumuelezea mkurugenzi mtendaji halmashauri ya Arusha, Seleman Msumi ( aliyevaa skafu) shughuli zinazofanywa na vikundi vya wajasiriamali wanaoishi na Virusi vya UKIMWI.

Mkurugenzi mtendaji halmashauri ya Arusha, Seleman Msumi akizungumza na hadhara wa wananchi, wakati wa maadhimisho ya siku ya UKIMIWI Duniani, yaliyofanyika kwenye viwanja vya Balbal kata ya Oloirieni halmashauri ya Arusha.


Makamu Mwenyekiti halmashauri ya Arusha, na Diwani wa kata ya Matevesi, Mheshimiwa Freddy Lukuma akizungumza na hadhara wa wananchi, wakati wa maadhimisho ya siku ya UKIMIWI Duniani, yaliyofanyika kwenye viwanja vya Balbal kata ya Oloirieni halmashauri ya Arusha.

Konga la WAVIU halmashauri ya Arusha wakisoma risala mbele ya mgeni rasmi, wakati wa maadhimisho ya siku ya UKIMIWI Duniani, yaliyofanyika kwenye viwanja vya Balbal kata ya Oloirieni halmashauri ya Arusha.


Mkurugenzi mtendaji halmashauri ya Arusha, Seleman Msumi akisiskiliza mawsilisho ya namna ukeketaji unafanyika, kutoka kwa wadau wa shirika la HMD, maonesho yaliyofanyika wakati wa maadhimisho ya siku ya UKIMIWI Duniani, yaliyofanyika kwenye viwanja vya Balbal kata ya Oloirieni halmashauri ya Arusha.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • DKT. PASCAL KATIKA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA

    June 19, 2025
  • WIKI YA UTUMISHI WA UMMA

    June 18, 2025
  • MAADHIMISHO YA WIKI YA UTUMISHI

    June 17, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.