• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

BENKI YA CRDB YAKABIDHI JENERETA HALMASHAURI YA ARUSHA KWA MATUMIZI YA OFISI

Posted on: August 19th, 2023


Benki ya CRDB imeikabidhi halmashauri ya Arusha Jenereta lenye ukubwa wa Kv 22 lenye thamani ya shilingi milioni 23.5, kwa ajili ya matumizi ya ofisi za halmashauri hiyo, jenereta ambalo hapo awali lilikuwa likitumiwa na benki hiyo tawi la Sekei, tawi ambalo kwa sasa limefungwa.

Akizungumza wakati wa hafla fupi ya makabidhiano yaliyofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa halmashauri ya Arusha, meneja wa CRDB kanda ya Kaskazini Bi Chiku Issa amesema, Benki ya CRDB imewiwa kutoa jenereta hilo kwa halmashauri kutokana na ushirikiano mzuri uliopo kati ya benki hiyo na uongozi wa halmashauri ya Arusha.

“Benki ya CRDB imekuwa na ushirikiano mzuri wa muda mrefu, hasa kwa kipindi chote ambacho Tawi la CRDB Sekei likifanya kazi katika eneo hili, Benki ilishirikiana na halmashauri katika mambo mbalimbali ya kuhudumia jamii, kimsingi  CRDB kama benki ya kizalendo imeunga mkono juhudi hizo za serikali". Amebainisha Chiku

Aidha ameongeza kuwa  Benki ya CRDB inachukulia kwa uzito suala la uwezeshaji wa wa utoaji huduma kwa wananchi kiseka, hivyo inaungana na serikali katika kusaidia jamii kupitia sera ya benki ya kusaidia jamii yaani 'Cooperative Social Responsibility Policy', sera ambayo inaelekeza Benki kutoa asilimia 1 ya mapato yake kila mwaka na kuyaelekeza katika kusaidia jamii kwenye nyanja za elimu, afya, mazingira na uwezeshaji wa mitaji kwa makundi mbalimbali ya kijamii.

Amefafanua kuwa, utoaji wa Jenereta ni mwendelezo katika kutoa huduma kwa jamii ili kuhakikisha wananchi wanahudumiwa wakati wote, hata pale itakapokuwa inajitokeza changamoto ya kukatika umeme kukatika shughuli ziendelee bila kukwama, na kushauri kuwa ile bajeti iliyotengwa kwaajili ya kununua Jenereta sasa inaweza kuelekezwa maeneo mengine kwaajili ya maendeleo ya jamii.

Akizungumza kwa niaba ya mkuu wa wilaya ya Arumeru, Mwenyekiti wa halmashauri ya Arusha Mhe. Dkt.Ojung’u Salekwa licha ya kuishukuru Benki ya CRDB kwa msaada huo wa Jenereta, ameweka wazi kuwa jenereta hilo ni muhimu kwa halmashauri hiyo, itakayosaidia kufanyika shughuli za utaji huduma kwa wananchi wakati wote, pindi itakapotokea changamoto ya kukatika umeme na kuahidi kuendelea kushirikiana nayo katika shughuli nyingine za kijamii.

“Kwa niaba ya mkuu wa wilaya, napenda kuwashukuru sana kwakuwa sasa hapatakuwa na kukwama kwa shughuli kwa ukosefu wa umeme, lakini yote hii ni kutokana na uhusiano mzuri tulio nao kati yenu na sisi, mmekuwa washirika wetu muhimu sana katika shughuli za maendeleo, ni jana tu mlitupatia madawati 50 yatakayosaidia watoto wetu kutimiza ndoto zao na tunacho angalia hapa siyo idadi ya madawati tunayopata, bali idadi ya watoto watakao yatumia. Madawati 50 maana yake mmewawezesha watoto 150 kujifunza huku wakiwa na utulivu”

Awali mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya Arusha, Seleman Msumi pamoja na kuishukuru Benki ya CRDB kwa msaada huo wa Jenereta, amebainisha kuwa Serikali kupitia halmasahuri inatambua mchango mkubwa wa benki hiyo katika kuwahudumia wananchi na kutimiza malengo ya Serikali.

“Tuna tambua jitihada zenu kama benki katika kuwahudumia wananchi wetu, mmekuwa mstari wa mbele kwenye masuala ya kijamii,  pale tunapowakimbilia kwaajili ya kushiriki kwenye mambo mbalimbali ya elimu na afya, na hii imejidhihirisha wazi leo, tulipowaomba kutuachia kitendea kazi hiki, kifua umeme hakukuwa na kigugumizi na hatimaye leo mmetukabidhi, tunawashukuru kuiunga mkono  Serikali ya awamu ya sita inayo ongozwa na Mh.Dkt Samia Suluhu Hassan katika kutekeleza Ilani ya Chama cha Mapinduzi”. Amesema Msumi

Hata hivyo baadhi ya watumishi wa halmashauri ya Arusha wameipongeza na kuishukuru benki ya CRDB kwa kuwapatia Jenereta na kuweka wazi kuwa, itarahisisha shughuli mbalimbali za utendaji kazi hasa kazi za mifumo pale inapotokea umeme umekatika.

 “Jenereta ni muhimu sana kwa taasisi yetu, kazi nyingi za kimfumo zinahitaji umeme, kunakuwa na ucheleweshaji wa kazi pale inapotokea umeme umekatika, kuwepo kwa jenereta na mbadala wa umeme, hivyo tunaahidi kuongeza ufanisi katika kazi za kuwahudumia wananchi". Amesema Mtumishi asiyetaka jina lake litajwe.


Arusha DC ni Yetu, Tushirikiane kuijenga

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • DKT. PASCAL KATIKA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA

    June 19, 2025
  • WIKI YA UTUMISHI WA UMMA

    June 18, 2025
  • MAADHIMISHO YA WIKI YA UTUMISHI

    June 17, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.