Na Elinipa Lupembe
Serikali imeendelea kuimarisha upatikanaji na utoaji wa huduma kwa wananchi, kwa kutoa fedha za kutekeleza miradi ya maendeleo katika halmashauri nchini, huku Halmashauri ya Arusha, ikiwa miongoni mwa halmashauri iliyonufaika kwa kupata fedha kiasi cha shilingi bilioni 3. 27 kutoka Serikali Kuu ikiwa ni fedha za utekelezaji wa bajeti ya mwaka wa fedha 2022/2023 ukioanza Julai 1, 2022.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi ofisini kwake Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha, Seleman Msumi, amethibitisha kuwa shilingi bilioni 3.3 zinatumika kutekeleza shughuli za mbalimbali za halmasahuri hiyo ikiwemo utekelazaji wa miradi ya maendeleo kwa kipindi cha robo ya kwanza ya kuanzia Julai - Septemba kwa mwaka wa fedha 2022/2023.
Msumi ametaja fedha hizo ni kuwa, kiasi cha shilingi bilioni 3.27 ni kutoka fedha kutoka Serikali Kuu na shilingi milioni 95.2 zikiwa ni fedha za mapato ya ndani ya halmashauri, na utekelezaji wake unaendelea kukamilika.
Aidha ameutaja mchanganuo wa fedha hizo kuwa milioni 658.4 fedha za elimu bila malipo wa idara ya msingi na sekondari huku milioni 227.9 elimu msingi na milioni 430 kwa elimu sekondari na kuongeza kuwa shilingi milioni 589.5 zikitumika katika utekelezaji wa ujenzi wa miundombinu ya shule pamoja na milioni 187.8 fedha za kuendesha shughuli za mitihani ya Taifa.
Katika sekta ya Afya serikali imetoa shilingi milioni 502.6, kwa mchanganuo wa milioni 52 kwa ajili ya shughuli za chanjo, milioni 50.6 fedha za Mpango wa Kudhibiti UKIMWI, milioni 50 ujenzi na ukamilishaji wa zahanati ya Mirongoine pamoja na milioni 350 kwa ajili ya ununuzi wa vifaa tiba.
Hata hivyo serikali kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) halmashauri imepokea kiasi cha shilingi 602, fedha kwa ajili ya walengwa 13, 920 walio kwenye mpango wa kunusuru kaya maskini.
Aidha mkurugenzi Msumi amefafanunua kuwa serikali imetoa shilingi milioni 760 nje ya bajeti kwa jaili ya ujenzi wa vyumba 38 vya madarasa kwa shule 15 za sekondari ikiwa ni maandalizi ya kupokea wanafunzi wa kidaato cha kwanza wanaotegemea kupangiwa kwenye shule za serikali kwa mwaka wa masomo 2023.
"Fedha zote hizo tayari zimetekelezwa kulingana na shughuli zilizopangiwa, huku utekelezaji wa miradi ya maendeleo ukitumia 'Force' Akaunti kwa kutumia mafundi wazawa chini ya usimamizi wa kamati za ujenzi zinazoundwa kisheria na wananchi wa maeneo husika" Amesisitiza Mkurugenzi Msumi
ARUSHA DC
KaziInaendleea ✍✍
MGAWANYO WA FEDHA NI KAMA UNAVYOONEKANA KWENYE JEDWALI MDUARA
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.